Wakati Kikwete Akiponda Uongozi wa Simba na Yanga, Mwanae Apewa Uongozi Yanga

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


DAKIKA chache baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete kuponda mfumo wa uongozi wa klabu kongwe chini zikiwemo Simba na Yanga, mtoto wake, Ridhiwani leo ametangazwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kitega uchumi cha Yanga katika eneo la makutano ya Mitaa ya Mafia na Nyamwezi, Ilala jijini Dar es salaam.

Kikwete akiwa katika uzinduzi wa kituo cha michezo cha Azam Complex huko Mbande Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, alisema viongozi wengi wa klabu hizo wapo kwa maslahi yao binafsi na si kuzinufaisha klabu.

“Hawa Azam hawana gozigozi katika utawala tofauti na klabu kubwa za hapa nchini na mimi nawaambia Azam sasa ni timu kubwa na inazisumbua sana hizo mnazoziita timu kubwa,” alisema Kikwete na kuongeza;

“Leo hii ninyi mna kituo cha kukuza vijana, wenzenu Simba na Yanga hawana kitu kama hiki, wamekalia ukiritimba tu siku zote na ndiyo maana hawafanikiwi.”


Kikwete aliyasema hayo leo mchana huko Mbande Chamazi, lakini katikati ya jiji la Das es Salaam kwenye makutano ya mitaa ya Jangwani na Twiga yalipo makao makuu ya Yanga, Mwenyekiti wa timu hiyo, Yusuf Manji alikuwa akimtambulisha Ridhiwani Kikwete kuwa mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kitega uchumi katika eneo la klabu lililopo makutano ya Mafia/Nyamwezi eneo la Ilala jijini Dar es salaam.

Manji alisema uteuzi wa Ridhiwani umezingatia uwezo wake kwa taaluma yake, na moyo alionao katika kujitolea katika kazi mbalimbali za klabu ya Yanga.

"Wote tunamfahamu Ridhiwani amekua ni mwanachama wa Yanga kwa muda mrefu, amekua akijitoa katika kazi mbalimbali za maendeleo ya klabu, hivyo tumeona ni vizuri kumpa fursa hiyo ili aweze kusaidia katika kuleta maendeleo ya klabu" alisema Manji

Katika kamati hiyo ambayo Ridhiwani ameteuliwa, amepewa fursa ya kuteua/kuchagua wajumbe atakaoshirikiana nao katika ujenzi wa kitega uchumi hicho, pia atakua na uwezo wa kuongeza wajumbe au kupunguza kulingana na mahitaji kwa kipindi hicho.

Mara baada ya kutambulishwa kwa wanachama na waandishi wa habari, Ridhiwani alisema anashukuru kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo na kuahidi kuwa atajitahidi kadri ya uwezo wake kuhakikisha ujenzi huo unafanikiwa.

"Nitakaa na kuangalia ni wajumbe gani ambao tutaweza kukaa pamoja na wajenzi (wakandarasi) ili kuweza kufanikiwa katika ujenzi wa kitega uchumi, kwani napenda eneo hilo liwe sehemu ambayo litasaidia katika uchumi wa klabu" alisema Ridhiwani


MASWALI TATA

Je, leo Kikwete amewaponda viongozi wa klabu kubwa nchini, na wakati huo huo mtoto wake anateuliwa kushika nafasi kubwa katika klabu, Ridhiwani ni mmoja kati ya viongozi waliopondwa?

Ridhiwani anaweza kumfanya baba yake ageuze au kupindua kauli yake aliyoitoa leo?

Je, maneno ya Kikwete yalihusiana na uteuzi wa Kikwete?

Au Kikwete alitamka bila kujua kama Ridhiwani amepewa uongozi Yanga?

Kazi kwenu!


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Inahu? Baba ni baba mtoto ni mtoto,kila mtu na mambo yake na mtazamo wake na maamuzi yake,kwani akiwa mwanae ndo nn!

    ReplyDelete

Top Post Ad