AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Chanzo cha habari kutoka ndani ya shirikisho hilo kililitonya Ijumaa kuwa, Mhe. Makalla alimvaa Mwakifwamba kwenye mkutano na wasanii uliofanyika ndani ya Hoteli ya Kibadamu, Ubungo jijini Dar.
“Mhe. Makalla ndiye aliyekuwa mgeni rasmi, akiwa pale alimuuliza Mwakifwamba kuhusu hatua walizochukua kwa Jack Chuzi baada ya kuandikwa habari kuwa alinaswa akienda kuuzwa.
“Mwakifwamba alijitetea kuwa, wanalishugulikia na Mwenyekiti wa Chama cha Waigizaji Tanzania, Michael Sangu ‘Mike’ akasisitiza kuwa, wako katika mchakato wa kulitolea uamuzi tukio hilo lililofanywa na Jack ,” kilidai chanzo hicho.
Baada ya kuzinyaka habari hizi paparazi wetu alimtafuta Mwakifwamba lakini hakuweza kupatikana mara moja ila Mike alipoulizwa juu taarifa za Mhe. Makalla kucharukia ishu ya Jack alisema:
“Ni kweli waziri aliuliza kuhusu hatua tulizozichukua kuhusu suala la Jack kujiuza ambapo nilimjibu kuwa tuko kwenye mchakato wa kulitolea uamuzi na kwa sasa tumeunda kamati maalum, ikimaliza uchunguzi wake ndiyo tutatoa jibu kuwa tumemchukulia hatua gani.”
Source:Global Publisher
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK