AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kwa mujibu wa chanzo chetu, tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo dada huyo alikodi Bajaj hiyo toka nyumbani kwake, Kinondoni-Shamba jijini Dar kwenda kujirusha katika klabu moja ya usiku iliyopo Mwananyamala ndipo alipolizwa pochi hiyo iliyokuwa na fedha (zaidi ya elfu hamsini) pamoja na vitambulisho.
Chanzo hicho kilizidi kueleza kuwa, kabla hajafika klabu, dada huyo aliamua kumpitia shosti yake aliyekuwa katika Baa ya Uhuru Peak, Mwananyamala ili wakajirushe pamoja ndipo dereva huyo alipomfanyizia.
“Alipofika hapa Uhuru Peak akaacha pochi yake ndani ya Bajaj ili amshtue fasta rafiki yake ndipo dereva alipotumia mwanya huo kutokomea kusikojulikana,” kilisema chanzo hicho.
Baada ya dakika kadhaa, dada huyo alitoka nje na kuanza kuangaza huku na huko ghafla akapata msala mwingine wa kutiwa mbaroni na Jeshi la Polisi lililokuwa katika msako wa kuwakamata machangudoa.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
wakome mke wa mtu usiotulia na mumewako inahusu! ukitoka uwe na mume. hukumu hapahapa duniani
ReplyDelete