Wasomi: Spika anavuruga Bunge

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kutoa mwongozo na kuunga mkono uamuzi wa Naibu wake, Job Ndugai kuwasimamisha wabunge sita wa Chadema, wasomi, wanasiasa na wanaharakati wamesema Kiti cha Spika ndiyo chanzo cha mvutano bungeni kwa kuwa kinapendelea wabunge wa chama tawala (CCM).

Wamesema licha ya Bunge kuongozwa na kanuni, wakati mwingine viongozi hao wa Bunge wanatumia kanuni hizo kuwapendelea wabunge wa CCM, huku wakieleza kuwa licha ya wabunge wa chama hicho kutukana, hawakupewa adhabu yoyote.

Jumatano ya wiki hii, Ndugai aliwasimamisha Tundu Lissu (Singida Mashariki), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiah Wenje (Nyamagana) na Godbless Lema wa Arusha Mjini kutohudhuria Bunge kwa siku tano kutokana na alichokiita kufanya vurugu ndani ya Bunge.

Uamuzi huo wa Spika Makinda ulikuja baada ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kumtaka Ndugai aeleze alitumia kanuni gani kuwasimamisha wabunge hao.

Licha ya wabunge hao kupewa adhabu hiyo baada ya kuomba mwongozo wa Spika na baada ya kupinga mwenzao kutolewa ndani ya ukumbi wa Bunge, wapo wabunge wa CCM waliotukana na kutoa lugha za kukera lakini hawakuchukuliwa hatua yoyote.

Wabunge hao ni Peter Serukamba ambaye alitukana tusi zito la nguoni kwa lugha ya kimombo wakati ulipozuka mzozo wakati wa hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Profesa Kulikoyela Kahigi.

Wengine ni mbunge wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia, Mwigulu Nchemba (Iramba Magharibi) na Livingstone Lusinde (Mtera).

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi Jumapili jana, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam, Profesa Gaudence Mpangala alisema, “Bunge la sasa linakabiliwa na mambo mawili makubwa; la kwanza ni udhaifu wa kiti cha Spika na pili ni wabunge wa CCM kuamini kuwa Chadema ni maadui wakati katika hali ya kawaida siasa ni ushindani na ndiyo demokrasia kwa kuwa sasa tuko katika mfumo wa vyama vingi.”

Alisema kuwa Spika na Naibu wake wameshindwa kudhibiti vurugu bungeni kwa sababu ya kuendekeza itikadi za vyama.

“Kushindwa huko ndiyo kunachangia vurugu kwa sababu wote wanaegemea upande mmoja, wabunge wengine wa upinzani hawawezi kukubaliana na hali hiyo na huo ndiyo mwanzo wa malumbano,” alisema Profesa Mpangala.

Alisema tatizo jingine ni kitendo cha wabunge wa CCM na chama chao kudhani kuwa upinzani ni uadui, “Hayo ndiyo matunda ya mfumo wa vyama vingi. Mfumo huu ni wa ushindani na kuna mambo ya msingi yanayotolewa na wapinzani na mengine hayana ubaya wowote.”

Mhadhiri mwingine wa Chuo hicho, Bashiru Ally alisema Spika anaongoza Bunge kwa ushabiki wa vyama; “Hatuwezi kutenganisha tabia za wabunge ndani na nje ya Bunge, ila pamoja na hilo bungeni sasa kuna ushabiki wa vyama.”
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad