AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wazazi waliamua kumsaidia mtoto wao, wakampa support yote, alijifungua salama mtoto wa kiume, na wazazi walimchukua mtoto yule akiwa na miezi mitatu, ili binti yao aendelee na masomo. Binamu yangu alimaliza shule na matokeo mazuri sana, alipata kazi, akajiendeleza zaidi na shahada ya uzamili. Hakupata bahati ya kuolewa lakini anamudu kumsomesha mtoto wake katika shule nzuri tu, na maisha yake na mtoto wake ni mazuri sana.
Kijana alitoka kwenye familia nzito, zengwe lilivyotokea, wazazi walimtafutia shule nchi za mbali, akakata mawasiliano na binamu yangu kabisa. Dunia ni duara, amekutana na baba wa mtoto, alimaliza shule na kuoa, yeye na mkewe wamebahatika kupata mabinti wawili, sasa kujua mtoto wa kiume aliye nae ni yule wa binamu yangu tu, anamsumbua sana kutaka mtoto wake, tena kwakuwa binamu yangu hana mume, anajiona anahaki ya kwenda kwake saa yeyote ile. Mpeni ushauri binamu.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
huyo ndg yako aache ufala
ReplyDeleteUshauri gani,mambo mengine ni kutumia common sense,akijilegeza imekula kwake na atakuwa fala sana
ReplyDeletemimi ushauri wangu ni huu mtoto ameshazaliwa na aliyemgaramia mtoto mpaka akakuwa ni wazazi wa binti kwa nini huyu anayeomba ushauri asiombe kwa wazazi wake ambao ndio wamemlelea huyo mtoto wakati binti yao akisoma hapa sijui imekakaaje hii au wazazi wa binti hawapo hai anyway mimi ushauri wangu ni huu baba ni baba tu siku zote haijalishi amemlea au vipi huyu mwenye kutaka mtoto wake alipe garama zoote kuanzia mtoto alipo zaliwa mpaka sasa akishalipa anaweza kumchukua mtotowake kwa maelewano lakini hili jambo liende mbele ya sheria maana sheri ni msumeno ni hayo tuasikubali amchukue kirahisi
ReplyDeletemimi ushauri wangu ni huu mtoto ameshazaliwa na aliyemgaramia mtoto mpaka akakuwa ni wazazi wa binti kwa nini huyu anayeomba ushauri asiombe kwa wazazi wake ambao ndio wamemlelea huyo mtoto wakati binti yao akisoma hapa sijui imekakaaje hii au wazazi wa binti hawapo hai anyway mimi ushauri wangu ni huu baba ni baba tu siku zote haijalishi amemlea au vipi huyu mwenye kutaka mtoto wake alipe garama zoote kuanzia mtoto alipo zaliwa mpaka sasa akishalipa anaweza kumchukua mtotowake kwa maelewano lakini hili jambo liende mbele ya sheria maana sheri ni msumeno ni hayo tuasikubali amchukue kirahisi
ReplyDelete