Chadema isitegemee kusifiwa na ccm hata siku moja.

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kiuhalisia chadema imekuwa msitari wa mbele katika kuuamsha umma juu ya matukio ya uhujumu uchumi unaotokea katika nchi hii kwa muda sasa na kufanya wananchi kuelewa kwa nini nchi hii ni maskini na viwanda vyote vimefishwa badala ya kuendelea na kujenga vingine vipya. Chadema ilichofanya si haba kwani hali ilivyo sasa hata katika vijiji ni hamasa tupu ya mabadiliko japo kuna watu wameketi huko waliko na kujifanya hawaoni hilo, huku katika vijiji vyetu vilivyo remote kabisa mambo yamegeuka kwa mfano katika vijiji vya huku geita ambako kutoka kijiji kimoja hadi kingine ni pori kubwa mambo si haba.

naomba nirudi kwenye topic: Kwa misingi hiyo niliyoeleza hapo juu ccm wanafanya kila lililo ndani ya uwezo wao ili kupotosha umma kuwa chadema ni chama cha fujo, kikanda, kikabila, udini na uhanaharakati. Kwa hali hiyo mimi binafsi napenda kuwashauri viongozi wa chadema kutokubali kucheza muziki wa ccm kwani muziki huo unahitaji mtu uwe umechanganyikiwa ndo uweze kwenda na hiyo beat. Kwetu sisi tuliokuwa kwenye ground tunajua hali halisi iliyoko huku.

Kwa kuanzia napenda kuwaasa viongozi wa chadema wamsome na kumuelewa nape ambaye alisifia mchakato wa katiba, ikumbukwe kuwa mambo yote yaliyo mabaya ccm huwa wanayasifia kwa kuwa ni wao waliyoyatengeneza kwa kulinda masilahi yao binafsi. Kwa hivyo chadema wanatakiwa suala hili walivalie njuga ili kutowapa muda wa kupumua kwani hata wananchi wenyewe wanaelewa ni nini kilichofanyika. Sisi tulioko huku vijijini tunaendelza kazi kama kawaida ya kumwaga sumu kwa wananchi, na tumefanya mkakati wa kuelimisha vijana wa sekondari kuelewa haya mambo kiundani zaidi.

Nisiwachoshe wasomaji na wachangiaji nitarudi tena kuendelea na nilichokimaanisha zaidi,
karibuni nyote..
Source:Mdau Jamii Forum
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad