Mtihani Mgumu kwa Rais Kikwete

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kuna kila dalili kwamba wabunge wa CCM wameanza kupanga majeshi kwa lengo la ‘kumalizana’ watakapokutana kwa siku mbili mfululizo na mwenyekiti wa chama hicho tawala, Rais Jakaya Kikwete.
Mkutano huo unaotajwa kuwa zao la jitihada za Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana unatarajiwa kufanyika kesho na keshokutwa mjini Dodoma, huku kukiwapo taarifa kwamba wabunge wamegawanyika katika makundi kwa lengo la kupenyeza, kisha kutetea hoja walizonazo dhidi ya wenzao.
Miongoni mwa hoja zinazotajwa ni ile ya kushughulikiwa kwa wabunge ambao wamekuwa wakitajwa kwamba ni wapinzani ndani ya CCM, wakiwamo, Alphaxard Kangi Lugora (Mwibara), Deo Filikunjombe (Ludewa), Ally Keissy Mohamed (Nkasi Kaskazini) na Luhaga Mpina (Kisesa).
Wabunge hao wanatuhumiwa na wenzao kwamba wanawasaidia wapinzani kutokana na misimamo yao ya kuikosoa hadharani Serikali katika vikao na mikutano tofauti ya Bunge.
Itakumbukwa kuwa Aprili 25 mwaka huu baada ya kukwama kwa Bajeti ya Wizara ya Maji, wabunge wa CCM walikutana katika kikao cha dharura kilichoongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambako Lugola na Filikunjombe walishambuliwa kutokana na kile kilichodaiwa kwamba wamekuwa wakiidhalilisha Serikali ya CCM bungeni.
Habari zilidai kwamba waliowashambulia wabunge hao ni wenzao, Saidi Nkumba (Sikonge) na Livingstone Lusinde (Mtera), huku wakitetewa na Beatrice Shellukindo (Kilindi) na Peter Serukamba (Kigoma Mjini) ambao walikaririwa wakisema kwa nyakati tofauti kwamba hawajakosea chochote kwani wanaeleza hali halisi ilivyo.
Baada ya mjadala huo, Pinda alikaririwa akimwelekeza Katibu wa Wabunge wa CCM, Janister Mhagama kumwandikia barua Katibu Mkuu wa CCM, Kinana kuhusu suala hilo ili liwe ajenda watakapokutana na Rais Kikwete.
Hata hivyo, kuna taarifa kwamba huenda hoja hiyo ikakosa nguvu kutokana na msimamo wa sasa wa Kinana ambaye anawaona wabunge wa CCM kama ni wapole, hali inayosababisha wale wa vyama vya upinzani hasa Chadema kupata nguvu.
Kutokana na hali hiyo, ni dhahiri kwamba Rais Kikwete atakuwa na wakati mgumu wa ama kukubaliana na hoja za wale wanaokosoa wenzao kwa kuikosoa Serikali au kuegemea upande wa Kinana ambaye kimsingi anaunga mkono ukosoaji unaofanywa na wabunge.
Harufu ya kile kinachodaiwa kuwa ni maandalizi kwa ajili ya mkutano huo ilianza kunukia jana pale Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipomtaka Lugola kuwasilisha ushahidi wa majina ya mawaziri aliodai kwamba wanajihusisha na biashara ya dawa za kulevya, ili ayafikishe kwa Rais Kikwete kwa hatua zaidi.
“Kila mtu anatakiwa aipime kauli yake kabla hajaitamka, kama Lugola ana ushahidi aulete mbele ya Bunge na tutayapeleka kwa Rais,” alisema Pinda wakati akijibu swali la Mbunge wa Tumbe, Rashid Ally Abdallah aliyesema anaamini hakuna waziri anayejihusisha na biashara hiyo kwani mchakato wa kuwapata hufanywa kwa umakini wa hali ya juu.
Abdallah alikuwa akirejea kauli iliyotolewa na Lugola mwezi uliopita kwamba atawasilisha bungeni majina ya watendaji wa Serikali wanaopokea rushwa ili kuficha majina ya mawaziri wanaojihusisha na dawa za kulevya na kwamba kauli hiyo ni nzito inayolidhalilisha Bunge.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad