Ngassa asaini Yanga miaka Miwili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Simba na Yanga zinakutana Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa mwisho kufunga msimu, huku Yanga wakiwa wamepania kulipa kisasi cha mabao 5-0.

Mechi hiyo ndiyo itakuwa ya mwisho kwa Ngassa ambaye mkataba wake umesainiwa bila kuwa na tarehe, Championi Jumatano limeshuhudia na lina uhakika asilimia mia.

“Mkataba na Ngassa kila kitu kimekamilika kama unavyoona, hapa tunachosubiri ni kuisha kwa msimu na mara moja atatua na kuanza kazi Jangwani,” alisema mmoja wa viongozi ambao huhusika na masuala ya usajili Yanga.

Alipoulizwa kwa nini mkataba huo ambao una saini ya Ngassa na dole gumba lake hauna tarehe, alijibu: “Bado hatujajua utaratibu wa TFF kama mkataba ukisainiwa kabla ya mwingine kuisha inakuwaje. Hatutaki kuingia kwenye matatizo na mtu.
“Kitu kizuri Ngassa baada ya mkataba wake na Azam FC kuisha, sasa ameamua kurudi nyumbani, nasi tumemkaribisha vizuri.”

Ingawa mhusika alifanya juhudi za kuficha eneo la malipo ya Ngassa lakini taarifa za uhakika zinaonyesha atakuwa analipwa dola 2000 (Sh milioni 3.2) kwa mwezi.

Kwa mshahara, Ngassa atakuwa mchezaji anayelipwa zaidi ya wachezaji wote Ligi Kuu Bara. Labda kama kuna timu kati ya Yanga, Simba au Azam FC itasajili mwingine na kumpa zaidi ya hizo.

Kwa misimu miwili Felix Sunzu amekuwa akiongoza. Analipwa dola 3,500 (Sh milioni 5.6), Mzambia huyo amemaliza mkataba na Simba, ataondoka. Wakati Ngassa akiwa Azam na Simba alikuwa anachukua Sh milioni 2 kwa mwezi.

Kuhusiana na fedha za usajili, kwa kuwa Ngassa ametua Yanga kama mchezaji huru, tayari ameshatanguliziwa ‘kishika uchumba’ cha Sh milioni 10 pamoja na gari aina ya Nissan Trail ambalo thamani yake inafikia hadi Sh milioni 23.

Ngassa amekuwa akilitumia gari hilo alilopewa na Yanga baada ya kuuza alilopewa na Simba aina ya Toyota Verrosa lenye thamani ya Sh milioni 16 kwa hofu ya kupokonywa na Simba siku atakaposema anakwenda Yanga.

Kuna taarifa kuwa Ngassa alisaini mkataba mwingine na Simba ambao angeanza kuutumikia baada ya mechi hiyo ya Jumamosi.

Simba kupitia kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Pope, imetangaza kwamba Ngassa alisaini mkataba mwingine wa mwaka mmoja, akapewa gari na fedha Sh milioni 30 na kama anataka kwenda kokote, basi atalazimika kurudisha fedha hizo.

Lakini Ngassa amekuwa akisisitiza hana mkataba na Simba na baada ya huo wa Azam FC iliyompeleka Simba kwa mkopo utakapomalizika, atakuwa huru kwenda anakotaka.

Ngassa ambaye yuko kambini na Simba mjini Zanzibar, amewahi kuliambia Championi kwamba kama Simba inamtaka abaki, basi lazima itoe kitita cha Sh milioni 150.


Habari na Saleh Ally
Chanzo - GLP
KIUNGO mwenye kasi, Mrisho Khalfan Ngassa, amerejea Yanga na kusaini mkataba wa miaka miwili kuichezea tena timu hiyo. Ngassa alianza kupata umaarufu mkubwa akiwa na Yanga kabla ya kuondoka na kujiunga na Azam FC kwa kitita cha jumla ya Sh milioni 98 na kuweka rekodi mpya ya usajili. Lakini Ngassa ameamua kusaini tena mkataba wake mpya Yanga wakati akiwa chini ya klabu ya Simba ambao ni watani wakubwa wa Yanga.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad