Obama Kuwasili Nchini Tanzania Julai Mosi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wakati Ikulu ya Marekani ikitangaza kuwa Rais Barack Obama anatarajiwa kuwasili nchini kwa ziara ya siku tatu kuanzia Julai Mosi hadi 3, Serikali ya Tanzania imesema ujio huo utasaidia kuinua uchumi kutokana na kufaidika na uwekezaji na misaada mbalimbali.
Rais Obama anatarajiwa kuzitembelea Senegal, Afrika Kusini na Tanzania.
Taarifa ya Ikulu ya Marekani iliyotolewa na Ubalozi wa nchi hiyo nchini, inasema Rais Obama atazuru Afrika kuanzia Juni 26 hadi Julai 3, ikiwa ni moja ya sehemu ya kuimarika uhusiano baina ya nchi yake na bara la Afrika.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma alisema ziara ya kiongozi huyo inatarajiwa kuinufaisha Tanzania maeneo ya biashara na uchumi.
Rais Obama ambaye ana asili ya Kenya ambako anatoka baba yake mzazi, baada ya kuchaguliwa kushika madaraka nchini mwaka 2009, alimwalika Rais Kikwete akiwa kiongozi wa kwanza kwenda Marekani kujadiliana masuala mbalimbali.
Ziara yake ya kwanza kwa bara la Afrika aliifanya nchini Ghana ambako alihutubia Bunge.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Acha aje bwana hawa ndio viongozi bwana sio wakina Mugabe na wenzake

    ReplyDelete
  2. Ni june bana umetudanganya

    ReplyDelete

Top Post Ad