Video Qeen Baby Candy Augua Malaria na Kudaiwa Amerogwa na Hasimu wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

VIDEO Queen wa Bongo Fleva, Mimah Mohammed  ‘Baby Candy’ ameibuka na kueleza namna ambavyo aliugua malaria kali hadi kudaiwa kuwa amerogwa na shosti wake, Jacqueline Pentzel.

Chanzo makini kililiambia Amani kuwa hivi karibuni nyota huyo alichanganyikiwa kwani majini huwa yanampanda kichwani mara kwa mara huku Jack  akidaiwa kuwa ndiyo chanzo cha matatizo hayo.
“Amewehuka kabisa, ukimuona utamuonea huruma na Jack ndiye anayedaiwa kumroga,” kilisema chanzo.
Baada ya habari hiyo kuvuja, paparazi wetu alimtafuta Baby Candy ambaye alikiri kuumwa pamoja kupata taarifa za uvumi kwamba Jack anahusika lakini yeye anamshukuru Mungu kwani ameshatibiwa hospitalini.
“Mimi na Jack bado tunaongea vizuri, niliamua kukaa mbali naye kwa sababu ya maneno mtaani, siwezi kusema alinifanyia kitu kibaya, nilikuwa nikisumbuliwa na malaria, nimetibiwa hospitali na sasa nimepona,” alisema.

Source:Global publisher
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad