Wakongo Watua Mazoezi ya Simba wakiwania Usajili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wakati Kocha mpya wa Simba, Abdallah Kibadeni akianza rasmi kazi ya kuifundisha timu hiyo, wachezaji 30 baadhi kutoka nchi za DR Congo na Msumbiji, jana ‘walivamia’ kambi ya mazoezi ya Wekundu hao wa Msimbazi kuwania kusajiliwa.
Wachezaji hao ni Joe Fils, Fabian Tshiyaz, Fabrice Baloko wanaotoka klabu ya Vita ya Lubumbashi ya DR Congo na Patrick Milambo kutoka Nguena FC pia ya Lubumbashi.
Wengine, Mohamed Abdallah wa klabu ya Ferreviario de Nampula ya Msumbiji, Adeyun Saleh (Miembeni) na Shaaban Kondo (Mbagala Jack Sports Academy).
Wanasoka wengine waliojitokeza kuwania kusajiliwa Msimbazi ni Rashid Salum (New Boko, Zanzibar), Ramadhan Kipiala (Buza), Shaaban Saidi (Boom FC) na Samuel Ngassa, mchezaji wa zamani African Lyon.
Wanandinga hao walijitokeza siku ya kwanza ya Kibadeni kuvaa mikoba ya Kocha Patrick Liewig kwenye Uwanja wa Kinesi.
Liewig alitimuliwa na uongozi muda mfupi baada ya kumalizika msimu wa Ligi Kuu Bara.
Akiongea kwenye Uwanja wa Kinesi jana, Kibadeni aliyewahi kucheza klabu hiyo na baadaye kuwa kocha, alisema angependa kufanya kazi kwa uhuru na bila kuingiliwa kwenye majukumu yake.
Kibadeni amesema, yeye kama kocha anafahamu wajibu wake katika kufundisha na kwa sababu hiyo, angependa kupata ushirikiano mzuri kutoka kwa viongozi wake.
“Hii ni mara yangu ya nne kufundisha Simba, wanachama na wadau wa soka wanajua jinsi gani nilivyokuwa naacha kazi, muda wote ilitokana na kukosa uhuru, kabla ya kujiunga na Kagera Sugar,” alisema Kibadeni.
Kibadeni alisema sababu kubwa ya kujiunga na Kagera ilitokana na hatua ya kocha wa Simba wakati huo, Moses Basena kutaja msaidizi wake awe pia kutoka nje na hivyo kumleta Richard Amantre.
“Kuna mambo ambayo kimsingi huwezi kuyakwepa hasa viongozi wanapoamua kufanya uamuzi fulani. Hili lilitokea wakati nafundisha Simba miaka ya nyuma,” alisema Kibadeni.
Kuhusu usajili, Kibadeni alisema: “Nimeikuta timu tayari ina mipango ambayo baadhi imeshatekelezwa. Ninachohitaji ni kufanya kazi na wachezaji wenye nidhamu nzuri.”
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad