Wema: “Ni kweli picha ni romantic lakini yule kijana (Raheem) si mpenzi wangu. Naomba nieleweke hivyo.”

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wema ambaye ni Miss Tanzania mwaka 2006, huku akifurukuta kwenye tasnia ya filamu za Kibongo, ametokelezea na mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina moja la Raheem katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
GUMZO MITANDAONI
Picha hiyo ambayo pozi lake ni ‘very romantic’ imezua gumzo katika mitandao mbalimbali ilipotundikwa na wadau wengi walionekana kuamini kuwa Wema alikuwa akimnadi mpenzi wake mpya.
Mtoa maoni mmoja aliandika: “Naona Wema ameamua kutuonesha shem wetu mpya, sasa hapo kazi kwa wenye vijicho.”
Mwingine aliandika: “Mmh! Mbona (Raheem) haonekani uso? Kama lengo lake lilikuwa kumwanika angemuacha tu aonekane ila dah! Ana kifua kizuri sana. Huyu jamaa anaonekana anafanya sana mazoezi.”
DIAMOND ATAJWA
Katika gumzo hilo, wengine walikwenda mbali zaidi, wakisema kwamba inawezekana Wema alikuwa na Raheem kwa siri muda mrefu lakini sasa ameamua kuvunja ukimya ili kumringishia x – boyfriend wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
“Siku zote alikuwa wapi? Atakuwa anamwoneshea Diamond tu huyu,” mtoa maoni mwingine aliandika.
INTERVIEW NA RAHEEM
Ni jadi ya magazeti ya Global Publishers likiwemo hili la Risasi Mchanganyiko kutafuta mzani wa habari kabla ya kwenda hewani hivyo lilimtafuta Raheem ambaye alitoa ushirikiano wa kutosha.
Raheem alikiri kuitambua picha yake na Wema lakini alisema imemshtua na kumcha-nganya maana hakutegemea kama ingefika mitandaoni na hatimaye kwenye vyombo vya habari.

Alisema: “Ni kweli nilipiga hiyo picha na Wema lakini ni ya kawaida tu, haina maana nyingine tofauti. Wema ni rafiki yangu na dada yangu. Tunaheshimiana, hakuna cha zaidi.
“Wema ni maarufu na watu wanaweza kujaji wanavyotaka, hilo litanisababishia matatizo kwa sababu mimi nina mpenzi wangu na Wema si mtu wangu kabisa…she is just my sister (ni dada yangu tu).”
Risasi: Hiyo picha mlipiga lini, wapi na kwa matumizi gani?
Raheem: Ilikuwa kwenye function (tukio) fulani ambayo siwezi kuizungumzia. Kama wiki sita au miezi miwili hivi iliyopita na tulipiga kama marafiki tu, hakuna cha zaidi.
Risasi: Kwa hiyo Wema akithibitisha wewe ni mpenzi wake itakuwaje?
Raheem: Nitamshangaa sana! Wema ni dada yangu tu.
Risasi: Inasemekana Wema ameamua kuianika hiyo picha kwa lengo la kumrusha roho Diamond, unasemaje hapo?
Raheem: Sijui na kwa kweli siwezi kuzungumzia mambo ya mtu binafsi. Sijui chochote.
GONGA HAPA KUMSIKIA WEMA
Wema alipatikana na kusomewa mashitaka yake ambapo alikiri kupiga picha na Raheem, akafafanua kuwa aliipiga muda mfupi baada ya kutoka kufanya interview na kituo kimoja cha redio (jina kapuni) lakini akasema haina uhusiano wowote na suala la mapenzi.
“Ni kweli nilipiga hiyo picha, yeye aliniomba tu kama fan (shabiki) wangu, akataka ku-show love (kuonesha upendo), sikuona sababu ya kumkatalia. Nakumbuka siku hiyo nilikuwa na Martin (Kadinda – meneja wake) na baada ya siku hiyo sijawahi kuonana naye tena mahali popote…sioni tatizo kabisa, ni kawaida kwa sisi mastaa,” alisema Wema.
Risasi: Lakini Wema wadau wanasema eti ni mpenzi wako na umefanya hivyo kwa lengo la kumrusha roho Diamond.
Wema: Umeshasema wadau, waache na mambo yao lakini maelezo yangu ni hayo na naamini yamejitosheleza.
Risasi: Kuna kitu nahitaji ufafanue zaidi…lile pozi lipo romantic sana, hufikiri kuwa inaweza kuwa sababu ya watu kuwa na hisia kwamba ni mpenzi wako?
Wema: Ni kweli picha ni romantic lakini yule kijana (Raheem) si mpenzi wangu. Naomba nieleweke hivyo. Ahsante
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hello! I understand this is somewhat off-topic however
    I had to ask. Does building a well-established website such as yours require a massive amount work?
    I am brand new to writing a blog but I do write in my journal
    everyday. I'd like to start a blog so I can share my experience and thoughts online. Please let me know if you have any recommendations or tips for brand new aspiring blog owners. Appreciate it!

    Feel free to visit my site metal vanity set with mirror

    ReplyDelete
  2. My dear you are asking the wrong person...cos the news in this blog are all copy pasted from other blogs (even the disclaimer says so)
    If u want real answers n real inspiring blogs u should direct ur questions to owners of blogs like the 8020fashion blog or the GPL blog (just to mention a few)

    ReplyDelete

Top Post Ad