LADY JAYDEE NA MWANAFA KESHO HAPATOSHI....SUGU AMPA SHAVU LADY JAYDEE NA ZITTO KABWE KALALA KWA MWANAFA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 Ile the Big Square 1, show za magwiji wa muziki Tanzania mwana FA ‘The Finest’ na Lady Jay Dee ‘Miaka 13 ya Lady Jay Dee’ zitapigwa kesho June 14, huku presha ikiwa inaongezeka hasa kwa fans wanaotamani kuhudhuria show walioichagua na kuona ukubwa wa show kama walivyotarajia.


Show hizi kubwa zina nguvu sana kutokana na ukubwa wa majina ya wasanii husika. Kwa mujibu wa lady Jay Dee timu anaconda kesho itaungwa mkono na mheshimiwa Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu.

Jide ambae hivi karibuni ameachia wimbo mpya unaopatikana kwenye album yake ‘Nothing but the truth’ inayoitwa Yahaya, amepost kupitia kupitia ukurasa wake wa facebook na pia katika akaunti yake ya Twitter kuonesha list ya wasanii watakaopanda jukwaani, na pia uwepo wa Sugu.

” Miaka 13 ya Lady JayDee, Ijumaa ya kesho shughuli inaanza rasmi saa 3:00 usiku...Ukiskia paaaa ujue show imeisha

1. Prof Jay 2. Juma Nature 3. Grace Matata 4. Hamza Kalala 5. Wakazi na ugeni wa Mh. Joseph Mbilinyi a.k.a SUGU

Nyimbo zote unazozipenda zitalia tar 14 June, pale Nyumbani Lounge sababu yaaaaa sababu yaaaaaa ?????????”

 Kwa upande wa Mwana FA ambae atapiga show yake na Live band akiwa na kundi kubwa na maarufu kwa upigaji wa Live Band ‘Wananjenje’, yeye amepewa full sapoti na mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto kabwe.
Zitto ameweka wazi kupitia akaunti yake ya twitter kuwa anamsapoti sana msanii huyo.

“You have my full support “@MwanaFA”
LeoT
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Wanaubaguzi mbona NGWAIR livyokufa waligairi lakn LANGA emekufa hawajasogeza mbele

    ReplyDelete
  2. hahahahaaa..... inategemea na haiba pia bro. Watu wengine si "fotogenik" kwenye gemu. kwenye msiba wa ngwair wasanii wa bongo movie na bongo fleva walifurika. Wiki iliyofata kafa muigizaji tukaona "umati" ulivyojitokeza. Ukifanya kazi kwa bidii na ukawa na upendo watu watakusindikiza bila kujali umekufaje. Wote ngwair na langa wamekula sembe mpaka zikawagharimu career zao na hata maisha ila ngwair aliji-identify na wabongo wengi ndo maana alipewa haki yake.

    ReplyDelete

Top Post Ad