MAREKANI YATOA ONYO KALI KWA MSAFARA WA RAIS OBAMA TANZANIA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Dar es Salaam. Licha ya ujumbe wa Rais wa Marekani, Barrack Obama kutarajiwa kufikia katika hoteli kubwa zenye hadhi wakati kiongozi huyo atakapowasili nchini Julai Mosi mwaka huu, Ikulu ya Marekani imetoa tahadhari ya vyakula ambavyo hawatakiwi kuvigusa wakiwa nchini ikiwa ni pamoja na kutumia maji ya bomba.
Mbali na tahadhari hiyo, ziara hiyo ya Obama itakuwa na ulinzi mkubwa ambao pengine haujawahi kutokea katika historia ya viongozi wa nje wanaotembelea Tanzania kwani utahusisha idadi kubwa ya magari, ndege za kijeshi na meli kubwa ya kivita ambazo zitakuwa zikifanya doria karibu na pwani ya Tanzania.
Tahadhari za matumizi ya chakula, maji na nyinginezo zimetolewa katika nchi zote tatu za Afrika ambazo Obama atatembelea, kila moja kwa jinsi Wamarekani hao wanavyoitathmini.
Rais Obama atatembelea nchi za Tanzania, Senegal na Afrika Kusini.
Ulinzi
Vyombo vya usalama vya Marekani vimejipanga kuhakikisha ziara ya kiongozi huyo haivurugwi kwa namna yoyote ile. Tayari ndege za jeshi zilizobeba magari ya akiba 56, yakiwemo 14 aina ya ‘Cadillac One’ maalumu kwa ajili ya kiongozi huyo, yamewasili katika nchi hizo tatu za Afrika atakazotembelea.
Kwa mujibu wa gazeti la Washington Post la Marekani, ndege hizo pia zimebeba malori matatu ambayo yamesheheni karatasi maalumu za kuzuia risasi kupenya kwenye vioo, zitakazobandikwa kwenye madirisha ya hoteli ambazo Rais Obama na ujumbe wake watafikia.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, mamia ya mashushushu wa Marekani tayari wako katika nchi hizo. Meli maalumu za kubeba ndege za kivita, maarufu kwa jina la ‘amphibious ship,’ ikiwa na hospitali maalumu na yenye vifaa vyote itaweka nanga baharini, jirani na nchi atakayokuwa Rais Obama, tayari kukabiliana na dharura yoyote itakayotokea. Gazeti hilo liliandika kuwa ndege za kivita za Marekani zitakuwa zikipeana zamu kufanya doria kwa saa 24, katika anga la nchi ambayo Rais Obama atakuwepo, iwapo ndege za ‘adui’ zitakaribia eneo linaloitwa ‘anga ya rais.’ Kwa mujibu wa gazeti hilo, ziara ya Rais Obama aliyoifanya hivi karibuni katika nchi za Ujerumani na Ireland Kaskazini, japo kulikuwa na gharama kwa walinzi, lakini safari za nchi za Afrika zimeelezwa kuwa na gharama kubwa zaidi.
Tahadhari
Kwa mujibu wa taarifa ya maelekezo ya Ikulu ya Marekani, ambayo Mwananchi imepata nakala yake, watu watakaokuwa kwenye msafara wa Obama wametakiwa kutotumia kachumbari. Pia imewataka kutumia maji ya chupa zaidi.
“Kutokana na mfumo wa maji uliopo, tunashauri watu wetu kutumia maji ya chupa zaidi kwa kunywa na hata kwa kupiga mswaki,” ilisema taarifa hiyo.
Kwa kuelewa fika tatizo la ugonjwa wa malaria nchini, ujumbe wa Obama umeshauriwa kutumia dawa ya mbu ya kupaka na kupuliza inayoitwa Deet.

Deet ni dawa maarufu huko Marekani na ikiwa katika aina tofauti ikiwamo ya kupaka na kupuliza na imekuwa ikitumiwa na jeshi la Marekani kwenye vita mbalimbali tangu miaka ya 1940 kabla ya kuanza kutumiwa na raia mwaka 1957.
ATM nazo noma
Pia watu watakaokuwa kwenye msafara wa Rais Obama wametakiwa kuhakikisha wanatumia mashine za kutolea fedha (ATM) zilizoko karibu na hoteli watakazofikia.
“Kuna tatizo la uhalifu kwa hiyo siyo vizuri kutumia ATM ambazo ziko katika sehemu zisizo salama. Pia katika kipindi watakachokuwa Tanzania watu wanapaswa kutumia teksi ambazo zimeidhinishwa na hoteli.
“Pia siyo vizuri kuacha kompyuta ya fedha kwenye vyumba mtakavyolala. Pia kina mama wanapaswa kuchukua tahadhari ya mabegi yao watakapokuwa wanapita mitaani,” ilitahadharisha taarifa hiyo.

Marekani yatoa onyo kali kwa msafara wa Rais Obama Da

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

16 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. ina maana nasis kikwete akienda ulinz unakuwa mzito hvyo?

    ReplyDelete
  2. Kikwete akienda marekani hata hakuna anayeshituka zaidi ya balozi wetu. Ni kama sisimizi akipita barabarani.

    ReplyDelete
  3. Hahahaa looo raisi wa Dunia

    ReplyDelete
  4. labda akienda arushaaaaaaaaaaa

    ReplyDelete
  5. dah hawa wa2 noma.kama kwa rais ni hivi je kwa mfalme ?.

    ReplyDelete
  6. SIONI TIJA YA HII ZIARA

    ReplyDelete
  7. acheni ufala waTanzania...Obama si MUNGU!

    ReplyDelete
  8. da.............,
    jamani,alie juu yupo juu tu,
    huyo anaesema anachukia americans just hizo ni propaganda zake ili nae aonekane,
    south africa pamoja na umafia wao wamefyata,
    ije kuwa sisi,
    tuongee tusiongee,ratiba ipo pale pale.
    hata wangekuwa kina HAO kama alivosema kakangu ,wangefyata tu

    ReplyDelete
  9. Maraisi wawili kwa mkuupuo so mchezo .Bush ni Rais na Pia mtoto wa rais

    ReplyDelete
  10. Safi sana kennytapawazi, sioni kinachofanya watu watoe maneno ya husda. Wa 2 havai moja hiyo itabaki kuwepo so kubalini matokeo. Ratiba ya ulinzi na usalama wa ziara iko palepale.

    ReplyDelete
  11. Sawa Haina shida atakama mneifuta comment yangu. Lakini Na nyie muwe wazalendo Au Ndo mnaogopa ukweli! Obama hajui Kiswahili Na ata JK akiziona izi comment hafanyi lolote.

    ReplyDelete
  12. Ivi Obama anakuja kufanya niñi Tanzania ? Je wamarekani wameooteza kiasi gani kwaajiri ya ziara yake ? Jiulize Na wewe. Watanzania tumekua tukiishia kushanikia kuja Kwa maraisi wakigeni nchini Mwetu huku hatujui kichafanyika huko ikuru Ni nini, hebu tasmini Ni mikataba mingapi yakisilisili imesainiwa? Watanzania tunatumia nguvu nyingi sana kutafuta kipato Kwenye ardhi yetu huku wachache walio wabinafsi wakila kiulaiiiiiiini Kwa mikataba yakisirisri Kama igwatavyo. Haya bwana kazi Ni Kwako 'Karibu mgeni mwenyeji niumie' nakupenda Tanzania

    ReplyDelete
  13. ah muna gas asilia nyny ndo mana atakuja kila raic mcjal na misaada itazd ili wakitaka gas muwape kwa bei ya buree

    ReplyDelete

Top Post Ad