Mchezaji Amri Kiemba Atua Yanga, Mkataba wake ni Kufuru

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

HATIMAYE aliyekuwa kiungo wa Simba, Amri Kiemba, amekubali rasmi kuachana na klabu hiyo na sasa atakuwa mchezaji wa Yanga msimu ujao.
Awali, Kiemba ambaye anatarajiwa kutua leo akitokea nchini Morocco alipokuwa na kikosi cha Taifa Stars, alikuwa na kigugumizi kizito juu ya kusaini mkataba mpya na Simba, kutokana  na Wekundu hao kushindwa kukubali dau alilotaka la Sh milioni 30 na mshahara wa dola 1,500 (sawa na Sh milioni 2.4).
Ofa hiyo ilionekana ngumu kwa Wekundu hao ambao walitaka kumpa Sh milioni 20 pekee nyota huyo ambaye aliifungia timu hiyo mabao saba katika Ligi Kuu Bara msimu uliopita.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo Championi Jumatatu limezipata kutoka kwa kaka wa kiungo huyo, Ulimwengu Hamim, tayari Kiemba ameshakubaliana na Yanga juu ya uhamisho wake, ambapo mara baada ya kutua leo, atasaini mkataba na klabu hiyo wenye thamani ya Sh milioni 35.
Ulimwengu ambaye pia ndiye Meneja wa Kiemba, alisema mbali na dau hilo, kiungo huyo atakuwa akichukua mshahara mnono wa dola 2,000 (sawa na Sh milioni 3.2), ambapo makubaliano hayo ameyafanya akiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Bin Kleb.
“Nilikwambia muda mrefu kwamba Yanga walikuwa wanamhitaji sana Kiemba, lakini mimi kama meneja wake niliwapa heshima sana Simba, niwe wazi, ofa ya Simba ilikuwa ndogo kulingana na mahitaji na thamani ya Kiemba na ndiyo maana tulishindwa kukubaliana,” alisema Ulimwengu na kuongeza:
“Tumekubaliana kila kitu, namsubiri Kiemba arudi huko kesho (leo), nafikiri jioni yake tutakutana tayari kwa tendo la kusaini mkataba mpya na Yanga utakaomfanya kuwa Yanga kwa miaka miwili, nadhani hilo sasa limekwisha.”
Kiemba ndiye mchezaji aliyekuwa akitumainiwa zaidi na Simba msimu uliopita. Kutua kwake Jangwani kunaifanya Simba iwe imepigwa bao mara mbili na Yanga. Awali Jangwani walimsajili beki Kelvin Yondani baada ya Wekundu kuonekana kuwa na kigugumizi juu ya kumsajili.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad