google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Rasimu yavuruga Mipango ya Urais 2015 | UDAKU SPECIAL

Rasimu yavuruga Mipango ya Urais 2015

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Dar es Salaam/Dodoma: Mapendekezo yaliyotolewa katika Rasimu ya Katiba Mpya na Tume ya Marekebisho ya Katiba yamewavuruga wanasiasa ambao tayari walikuwa wamejipanga kwa ajili ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Mwananchi limebaini.
Tangu juzi Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba alipotangaza rasimu hiyo, kumekuwa na wasiwasi mkubwa sasa kwamba mipango ya urais wa 2015 itavurugika ikiwa mapendekezo hayo yatapitishwa.
Tishio kubwa katika rasimu hiyo ni pendekezo la kuwapo kwa Serikali ya tatu hali ambayo inatafsiriwa na baadhi ya wanasiasa kwamba inaondoa nguvu ya Rais yeyote; awe wa Jamhuri ya Muungano, Zanzibar au Tanzania Bara.
Habari za kuaminika zilizopatikana kutoka ndani ya kambi za vyama vya CCM na Chadema zinaeleza kuwa wale waliokuwa wakifikiria kuwania nafasi hiyo wameingiwa na wasiwasi.
Kadhalika, suala la umri wa kuwania urais kubakia miaka 40 pia linaonekana kuwagusa waliowahi kutangaza kutaka nafasi hiyo ya juu ya uongozi wa nchi kabla ya mapendekezo ya tume.
Katika suala la urais, wanasiasa wenye nia hiyo wanauona uongozi wa Jamhuri ya Muungano kuwa ni kama hauna nguvu tena kutokana na kushughulikia mambo machache, lakini wakati huohuo wanauona urais wa Tanzania Bara kwamba hauna mamlaka kamili ya kuwawezesha watambuliwe nje ya nchi.
Tume ya Marekebisho ya Katiba imependekeza mambo saba tu yawemo chini ya Serikali ya Muungano kati ya 22 ya sasa. Yanayopendekezwa ni Ulinzi na Usalama, Katiba na mamlaka ya Jamhuri ya Muungano, mambo ya nje, sarafu na Benki Kuu, uraia na uhamiaji, usajili wa vyama vya siasa, ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na Muungano.
Ndani ya CCM
Makundi mbalimbali yanayowania urais ndani ya CCM inaaminika hayajafurahishwa na mapendekezo ya rasimu ya kutaka Serikali tatu.
Kwa maneno mengine, wanaona kama Rais wa Muungano ameng’olewa baadhi ya meno na masuala mengi yatakuwa yanashughulikiwa na Serikali ya Tanzania Bara na ile ya Zanzibar.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeliacha hewani suala la Tanganyika hasa baada ya kutoa mapendekezo ya Serikali tatu kwenye Rasimu ya Katiba.
Sitta ambaye ni Mbunge wa Urambo Mashariki (CCM), alisema hakuna mantiki ya kuunda Serikali tatu ikiwa Tume haikutoa mwongozo wa hali itakavyokuwa kwa Tanzania Bara, Serikali ya Muungano na ile ya Zanzibar.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad