SIRI YAFICHUKA.... CHADEMA WATHIBITISHA KUTUMIA MITAMBO MAALUM YA DVR KUMNASA MLIPUAJI WA BOMU LA ARUSHA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Imethibitika kwamba technology ya mawasiliano hivi sasa imekua kwa kasi ya ajabu sana, kiasi chakufikia kuwa kumbe siyo lazima tutegemee camera za waandishi wa habari kuchukua matukio.

Ni kwamba chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kwenye mkutano wake wa mwisho licha ya kutumia SATELLITE kurekodi mikutano yake, imethibitika kuwa chama hicho kilitumia mtambo maalum wa mawasiliano kurekodi mkutano wake wa mwisho katika uwanja wa soweto Arusha. Mtambo huo ambao unauwezo wa kurekodi matukio kwa masaa 72 mfululizo bila kuhitaji chaji, ulifungwa sehemu maalum ili kuweza kunasa matukio yaliyokuwa yanaendelea kwenye mkutano.

Mtambo huo ulisaidia kunasa tukio la mlipuko wa bomu na matumizi ya risasi kwenye mkutano kuwapiga raia, ambapo ulionyesha askari polisi aliyesimama pembeni ya nguzo ya umeme karibu na mfereji ulio mkabala na round about iliyo karibu na soweto garden akiwapiga risasi watu waliokuwa wanamkimbiza mtu aliyevaa suruali ya jeans aliyekimbia nakuingia kwenye gari ya polisi na kuondoka kwa kasi kwenye eneo la tukio. Mtambo pia uliweza kuonyesha gari ya blue landcruiser iliyoweza kui escort gari ambayo amepanda tule mtu aliyekuwa anakimbizwa.

Ule mtambo ambao una uwezo wa kurekodi matukio kwa around 360 degree angle uliweza kuonyesha tukio la watu wanaosadikiwa kuwa maaskari kufika kwenye eneo la tukio hasa kwenye gari la matangazo la chadema majira ya usiku, na kuweza kuzurura pale bila kuonyesha kwa kina walichokuwa wanakifanya pale.

video inaonyesha ule mtambo ulizima wenyewe saa moja na madakika asubuhi ya siku ya pili.

Kwa ujumla mtambo una taarifa nyeti za kuweza kusaidia kwa ushahidi wa tukio hili ambalo limegharimu maisha wa watu wasiokuwa na hatia. Muda utakapofika nadhani kwa idhini ya mwenyekiti wa chama kila kitu kitawekwa wazi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

13 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hiyo ndo itakuwa staili ya Chadema wakiingia madarakani. Hawatatumia vyombo vya dola vilivyopo kisheria kutoa suluhu ya matatizo!!! Sinema ndo inaanza sijui itaishia wapi???!!!!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kwani vyombo vya sheria ndio suluhisho la matatizo yote wewe msenge nini. Ingekuwa ndio suluhu mbona waliomtesa Ulimboka na Kibanda au waliomlisha sumu Mwakyembe wangeshakamatwa. Sheria anatunga binadam tu na anaweza kuwa msenge kama wewe kwa hio utekelezaji wake unakua mgumu. Vyombo havibagui kitu ukipigwa picha basi ukweli unabaki ukweli.

      Delete
  2. Sibuka kwa dola na miguvu isiyo na sababu kuzuia democrasia.

    ReplyDelete
  3. Hahahahaaa nilisema ccm bado washamba sana wanafikiri tz ya Mwl.bado ipo ila bila ushabiki tujifikilia hata sisi kwann ccm na serikali inawatetea polisi kwani ccm na serikali wanahofu nini maana wao si watuhumiwa inayotuhumiwa hapa ni polisi,,

    ReplyDelete
  4. Uwiii naihurumia ccm ya nape nawiye,,,na mwiguru kasomea ugaidi ataua chama hafai nawaambia wana ccm wenzangu hapa tuache ushabiki ,,viongozi wetu wamekosa mbinu nzuri za kuifanya ccm kuwa bora,,matamushi ya pinda ni dalili Tosha ya kukosa busara,kama kiongozi unaruhusu askari kutumia nguvu ikibidi siraha watumie,,mimi sipati picha ,,ukiua unaotaka kuwaomba kura utamtawala nani na kwa amani ipi,,,uvccm tuwe macho na hawa wazee wamezidiwa maarifa,,nape na mwiguru ni vijana ila mawazo ya yanaenekana ya kulewa madaraka

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tatizo wamezowea kubebana hata wakilopoka hawawajibishwi hao magamba,ndiyo maana wanaamua wanavyotaka kama mtoto wa mkulima alivyosema jana bungeni, is not fair, mm namshauri asiingie kanisani kabla ya kutubu.

      Delete
  5. Linda kauli yako inaonekana unataka vita ila kumbuka ,,,,usishangilie vita utakuja itafuta amani hutoiona tena

    ReplyDelete
  6. Haya yalitokea zanzibar wakamsingizia kukamatiwa wa watu ila Allah hamfuchi mnafiki atamfuchua hapahapa duniani na mkayapeleka katika dini sasa na hili mbona hamlipeleki kwenye dini au kwa sababu halijatokea zanzibar maana ndio wabaya wenu mkawaita mpaka nafasi nyama nyinyi sasa mnajua kipi kinachoendelea kudadadeki hata Bado

    ReplyDelete
  7. pinda umechemsha kauli yako unaonyesha kuzidiwa maarifa na wapinzani. Unatupa hofu wafuasi wako, futa kauli mkuu mbona unajiharibia? Hata wewe?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hiyo nafasi haiwezi tangu kitambo,tatizo ni kuwekana style.

      Delete
  8. pinda umechemsha kauli yako unaonyesha kuzidiwa maarifa na wapinzani. Unatupa hofu wafuasi wako, futa kauli mkuu mbona unajiharibia? Hata wewe?

    ReplyDelete
  9. pinda umechemsha kauli yako unaonyesha kuzidiwa maarifa na wapinzani. Unatupa hofu wafuasi wako, futa kauli mkuu mbona unajiharibia? Hata wewe?

    ReplyDelete
    Replies
    1. hapa nilipo natumia hiyo DVR pamoja na camera 36 ambazo zinapiga picha na kurecord matukio muda wote. Ni teknolojia ya siku nyingi sana ingawa hapa kwetu wananchi wengi hawajaitambua, kwa hiyo linalosemwa na CHADEMA linawezekana kabisa; ni teknolojia inayotumika na watu, asasi na kampuni nyingi nchini na dunia nzima kwa ajili ya pamoja na mambo mengine lakini hasa security.

      Delete

Top Post Ad