Yanga Yavuliwa Ubingwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Yanga ndiyo mabingwa  watetezi wa kombe la Kagame
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo  imesema kuwa haiwezi kuziruhusu timu za Tanzania  kushiriki katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika
Mashariki na Kati kutokana na hali ya usalama ya Darfur.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri, Amos Makalla baada ya gazeti hili kutaka kujua hatima ya timu za ushiriki wa timu za Tanzania katika mashindano hayo  yanayotarajiwa kufanyika wiki ijayo.
“Nipo kwenye kikao cha baraza la mawaziri, hata hivyo  hatuwezi kuziruhusu timu zetu kwenda eneo ambao si  salama, pamoja na kusubiri taarifa rasmi kutoka kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,”  alisema Makalla.
Kauli hiyo inaifanya timu za Yanga kupoteza ubingwa  wake, huku Simba na Super Falcon kuachana na  mashindano hayo kutokana na sababu hiyo muhimu. Timu hizo pamoja na Shirikisho la Soka nchini, TFF lilikuwa  linasubiri taarifa rasmi kutoka serikalini.
Awali, Rais wa Shirikisho la Kandanda nchini, TFF,  Leodegar Tenga alisema kuwa wao hawana taarifa zozote   kuhusiana na uamuzi wa Serikali zaidi ya kauli yao ya  kwanza.
“Sina taarifa, labda wewe  una taarifa rasmi kuhusiana na uamuzi  wowote kuhusiana na hatima ya timu za Tanzania
katika mashindano hayo,” alisema Tenga ambaye pia ni  Rais wa Cecafa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe alisema kuwa hali ya usalama wa Darfur si nzuri na kuiomba TFF ifikirie upya uamuzi wa upeleka timu Darfur kwani kuna ushahidi kuwa hali ya usalama si nzuri.
“Tuna ushahidi kuwa hali ya Darfur siyo nzuri kiusalama,  tumewaandikia TFF kuwaeleza hayo na kuwaomba  wafikirie upya ushiriki wa Tanzania katika mashindano  hayo,” alisema Membe.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad