DIAMOND AANIKA JUMLA YA MAPATO YAKE ALIYOINGIZA KWENYE SHOW ZA MWEZI ULIOPITA WA JUNE

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 
Staa wa Kesho, Diamond ameendelea kupiga hela kwa show nyingi zinazomfuata kila kukicha. Wingi wa show hizi unazidi kumfanya kuwa miongoni mwa wasanii wachache wa Tanzania wenye pesa nyingi zaidi.


Tumejaribu kuangalia baadhi ya show alizofanya mwezi huu, atakazofanya mwishoni mwa mwezi huu na mwezi ujao ili kukadiria ni kiasi gani anaweza kuwa ameingiza. Baadhi ya show tunafahamu ni kiasi gani aliingiza huku zingine tukikadiria kutokana na jinsi anavyochaji.
Show ya nchini Comoro 22 June
Katika show hii alisema alilipwa si chini ya dola 25,000 za kimarekani ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 38.
Show za Usiku wa wasafi Tabora 28 na 29 June
Mara nyingi katika show za ndani Diamond hachukui si chini ya shilingi milioni 10 kwa show mbili huenda akawa amelipwa zaidi ya shilingi milioni 15.
Show ya Tigo Mwanza 30 June
Katika show za makampuni kama hizi Diamond hulipwa si chini ya shilingi milioni 10.
Kili Music Tour 2013
Tulipata taarifa kuwa Diamond atafanya show kwenye mikoa minne na kwamba amelipwa shilingi milioni 50 kwa show zote.
Show ya Matumaini 7 July
 kwenye hii show diamond ana zaid ya mil.10

Show ya Kenya 27 July

Kwenye show hii Diamond atashare stage na mastaa wa Nigeria, Ice Prince na Davido na hapa kama alivyosema kuwa katika show za nje ya nchi huwa hachukui chini ya dola 15,000. Kuna uwezekano hapa akawa amelipwa zaidi ya shilingi milioni 20.
Kama una calculator basi unaweza ukapiga hesabu mwenyewe ni kiasi gani ameingiza kwa show za June na July. Kumbuka pia kuwa show zote hata za July tayari ameshasaini mkataba na ameshalipwa chake tayari. Kitu kama milioni 140 na usheee!!
Pia kumbuka ni balozi wa Cocacola na hulipwa kila mwezi kwa shughuli zinazohusiana na deal hiyo. Katikati wa mwezi July pia kuna uwezekano akawa na show zingine kibao.
“Siku zote ishi ukikumbuka, Maisha ni Vita, vita ambayo mwisho wake ni siku ya wewe kuingia kaburini, hivyo haupaswi kuchoka wala kukata tamaa.Heshima, Juhudi na Maombi ndio nguzo pekee zitazokusaidia wewe kushinda Vita hii… tambua Mwenyezi Mungu ndiye Muweza na Mpaganga wa yote,” anasema Diamond.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad