HATIMAYE MBOWE AJISALIMISHA POLISI

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

*Ni baada ya kusakwa siku kadhaa
*Ahojiwa kwa tuhuma za uchochezi

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amejisalimisha polisi. Mbowe, alijisalimisha polisi jana saa 8.00 mchana makao makuu ya Polisi Dar es Salaam na kuhojiwa na kikosi maalumu cha makachero wa jeshi hilo.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willbrod Slaa, alithibitisha Mbowe kujisalimisha polisi akiwa amefuatana na mwanasheria, Nyaronyo Kicheere.

“Si kweli kwamba Mbowe amekamatwa, amekwenda polisi mwenyewe. Kama nilivyoeleza kwenye mkutano wetu pale Manzese juzi…Polisi walikwenda nyumbani kwake Mikocheni usiku kwa ajili ya kumkamata hawakufanikiwa.

“Siwezi kusema anahojiwa au vipi, bali ameenda huko kama tulivyokubaliana,” alisema Dk. Slaa.

Hatua ya Mbowe kujisalimisha imetokana na tarifa kuwa polisi walivamia nyumbani kwake saa 6.00 usiku Ijumaa iliyopita kwa lengo la kumkamata.

Chanzo cha kuaminika kutoka makao makuu ya polisi, kilisema Mbowe alihojiwa kwa tuhuma mbalimbali zikiwamo za uchochezi anaoufanya kwa kujenga chuki kati ya wananchi na polisi.

Chanzo hicho kilisema tuhuma nyingine ni kauli yake aliyowahi kuitoa kuwa polisi inahusika katika tukio la mlipuko wa bomu uliotokea Juni 15 mwaka huu CHADEMA walipokuwa wakihitimisha mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo kwenye viwanja vya Soweto mjini Arusha.

Katika tukio hilo,watu wanne walikufa na wengine kadhaa kujeruhiwa vibaya katika tukio hilo.

Katika tukio hilo,Mbowe alidai Chadema kina ushahidi wa kutosha kuwa polisi wanahusika na tukio hilo kutokana na kuwa na mkanda wa video unaoonyesha tukio zima.

Lengo la kufanya hivyo linadaiwa kuwa ni kukidhoofisha chama hicho na kukisaidia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa madiwani Arusha.

Tuhuma nyingine ambayo Mbowe alihojiwa ni kuhusiana na kauli yake kuwa kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kutohudhuria mazishi ya watu waliofariki dunia katika mlipuko huo,kilihusishwa moja kwa moja kuwa ni ishara ya jeshi hilo kuhusika katika mauaji hayo.

Habari zaidi zinasema Mbowe anatuhumiwa kulichafua Jeshi la Polisi la Tanzania kwa kile alichodai ni moja ya jeshi katili Afrika Mashariki.

Chanzo chetu kilisema tuhuma nyingine ni uchochezi anaoufanya kuhusiana na kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyoitoa bungeni hivi karibuni.

Katika kauli hiyo, Pinda alisema alilielekeza jeshi la polisi kuwashughulikia watu wasiotii sheria.

Source:Mtanzania
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad