NGONO ZEMBE SEHEMU ZA KAZI-WANAWAKE HATARINI KUPATA MAGONJWA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kwa miaka mitatu iliyopita, Rehema Nduguru (50) anayeishi Mkoa wa Njombe alikuwa katika mazingira hatarishi ya kupata magonjwa ya ngono ikiwamo Ukimwi kutokana na kazi yake ya uhudumu wa baa.
Akitoa maelezo yake jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Rehema anasema kutokana na kazi hiyo alikuwa akilazimika kufanya ngono zembe ili kujiongezea kipato. Hata hivyo, anashukuru Mungu hakupata maambukizi ya Ukimwi.
“Wakati tukifanya kazi hiyo, mimi na wenzangu tulikuwa tukifanya ngono zembe, hasa na madereva wa magari ya mizigo yanayoegeshwa karibu na baa tulizokuwa tukifanyia kazi,” alisema Rehema.
Hata hivyo, Rehema sasa ameachana na kazi hiyo na amepata msaada kutoka Shirika la Kazi duniani (ILO).
“ILO walikuja Njombe na kutushauri tuunde vikundi ambapo tulipewa fedha zilizotuwezesha kufanya kazi zenye staha. Sasa ninauza nguo sokoni na ninapata fedha za kutosha kutokana na biashara hiyo. Tumeanzisha ushirika wa kuweka na kukopa (Saccos) ambayo inatuwezesha kujiendeleza kiuchumi,” anasema.
Kwa upande wake Mwajuma Sabuni anayefanya kazi katika kiwanda kimoja jijini Dar es Salaam (jina linahifadhiwa) analalamikia unyanyasaji wa kijinsia kutoka kwa waajiri wao.
“Nimefanya kazi katika kiwanda hiki kwa miaka saba sasa. Kwa miaka miwili ya awali nilifanya kazi kama kibarua, lakini baadaye nikaingizwa kwenye mkataba wa kazi na kuanza kukatwa mafao ya uzeeni na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), bila kupewa kadi ya uanachama na mwajiri wangu. Hadi sasa sijui hatima ya pensheni yangu,” anasema na kuongeza:
“Kwa jumla hali ya ajira katika kiwanda hiki ni ngumu hasa sisi wafanyakazi wa kike kwani rushwa ya ngono iko nje nje. Wasimamizi wa vitengo ndiyo wahusika na ukiwakataa ajira yako inakuwa hatarini. Licha ya kuwepo kwa Chama cha Wafanyakazi (Tuico) kinachojua kero zote hizi, bado hazijashughulikiwa. Naiomba Serikali iingilie katika kwa kuchunguza madai haya kwani tunanyanyasika mno.”
Maelezo ya wanawake hawa yanawakilisha kilio cha wafanyakazi wengi wanaonyanyaswa kijinsia kutokana na kazi zao. Wengi hulazimika kujiingiza kwenye ngono zisizo salama, hivyo kuhatarisha maisha yao hasa kwa kupata ugonjwa wa Ukimwi.
Katika mkutano wa wadau wa kupambana na ugonjwa wa Ukimwi, hasa maeneo ya kazi uliofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam, wadau wanasema kuwa wanawake na wasichana wako kwenye hatari zaidi ya kuathirika na ugonjwa huo na kwamba hatua stahiki zinapaswa kuchukuliwa ili kukabilia na tatizo hilo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids), Dk Fatma Mrisho anasema kuwa makundi ya wanawake walijitokeza kuomba msaada ili kujikwamua kimaisha na kujilinda.
“Hatari ya wanawake hawa kuathirika na Ukimwi ni kubwa mno. Ni changamoto kubwa inayohitaji jitihada za kila mmoja wetu,” anasema Dk Mrisho.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad