SKENDO YA WASANII KUSAFIRISHA UNGA KIMENUKA-CHRISTIAN BELLA AHOJIWA KWA MASAA MAWILI

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

KIMENUKA! Ile skendo ya mastaa kudaiwa kusafirisha madawa ya kulevya ‘unga’ imechukua sura mpya baada mwanamuziki wa dansi, Christian Bella ‘kutaitiwa’ uwanja wa ndege kwa takribani saa 2, Ijumaa Wikienda lina mkoba kwapani.
Bella alikutwa na ‘sheshe’ hilo hivi karibuni alipotua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar akitokea Sweden.
Bella alitua na ndege ya Shirika Uturuki ‘Tukish Airways’ majira ya saa nane na dakika 8, usiku mnene akiwa na mafurushi kibao huku akionekana na kitambi kilichodaiwa kuwatia shaka wanausalama ambapo alikaguliwa na mizigo yake kwa mitambo maalum.
 Paparazi wetu aliyekuwa eneo la tukio alimshuhudia Bella akizunguka kwenye mitambo ya ukaguzi huku abiria wengine wakimpita na kuruhusiwa kuondoka.
Huku familia yake ikipata hofu na kupigwa na baridi, ilipotimu mishale ya saa 10:00 alfajiri ndipo Bella alipomaliza kukaguliwa na kutoka kwenye mlango wa abiria wanaowasili kisha kupokelewa na Mkurugenzi wa Bendi ya Diamond Musica, Ally Ocs ‘Didik One’ ambaye amemsajili kwenye bendi yake.
Akizungumza na mwanahabari wetu kwa sharti la kutotajwa jina, mmoja wa maofisa wa usalama uwanjani hapo alisema: “Siku hizi madawa ya kulevya yamekuwa yakipenyezwa sana kwenye viwanja vya ndege hivyo hakuna mtu yeyote anayeaminika.
“Watu wanatumia njia mbalimbali, wengine wanameza, wengine wanaweka kwenye mizigo ndiyo maana mitambo yetu ilikuwa ikimsachi vizuri kila mtu na hasa huyo Bella ambaye kwanza alionekana kuwa na mafurushi mengi ‘then’ ametunatuna tumboni lakini bahati nzuri alipita salama kwenye mitambo yetu.”
Hata hivyo, jamaa huyo alitoa tahadhari kwa mastaa waosafirisafiri nje kuwa kama ishu hiyo wanaifanya waache kwa sababu wakikatiza eneo hilo lazima ‘kiwanukie’.
Baadhi ya mastaa wanaotajwa kupenda kusafiri nje ya nchi ni pamoja na Khadija Shaibu ‘Dida’, Khaleed Mohamed ‘TID’, Ali Kiba, Jacqueline Patrick na wengine kibao.
Kwa upande wake, mwanamuziki huyo alisema yeye anachojua viwanja vyote vya ndege kukaguliwa ni jambo la kawaida.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad