TEAM YA TAIFA STARS MGUU NJE, NDANI CHAN

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mfupa wa Waganda bado mgumu kwa Taifa Stars. Ni baada ya jana timu hiyo ya Tanzania kushindwa kufurukuta mbele ya wageni wao kwenye mchezo wa kwanza wa kufuzu kushiriki fainali za Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN) kufuatia kipigo cha bao 1-0.
Kwa matokeo hayo, Stars inahitaji miujiza kushinda mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo kwenye uwanja ambao utaamuliwa baadaye na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), kati ya Namboole au Nakivubo.
Katika mchezo huo kwenye Uwanja wa Taifa, Taifa Stars ilitawala sehemu kubwa ya kipindi cha kwanza na kuwapa wakati mgumu Uganda, lakini cha kusikitisha ni washambuliaji wake kukosa magoli yasiyo na idadi.
Bao pekee la Uganda lilifungwa dakika ya 46 kupitia kwa Iguma Dennis aliyemfunga kipa Juma Kaseja kwa shuti la pembeni ya lango akimaliza pasi ya shambulizi la kushtukiza kutoka kwa Mpande Joseph.
Kwa matokeo hayo, Stars inaendelea kuwa mteja wa The Cranes, na sasa ili isonge mbele itahitaji ushindi wa mabao 2-0 katika mechi ya marudiano.
Washambuliaji, John Bocco, Amri Kiemba, Mrisho Ngassa waliinyima Stars mabao mengi ya hasa kipindi cha kwanza walichotawala sehemu kubwa ya mchezo.
Uganda waliokuwa wakitumia nguvu nyingi kufika lango la Stars, hawakupata nafasi nyingi za kufunga, lakini nafasi moja waliyoipata ambayo haikuonekana kuwa ya hatari, ndiyo iliyowapa bao pekee.
Stars walikuwa wa kwanza kupiga hodi lango la Uganda dakika ya kwanza, baada ya krosi ya John Bocco kushindwa kuunganishwa wavuni na Amri Kiemba aliyekuwa kiasi cha mita tano kutoka langoni.Mrisho Ngassa aliyekuwa akiwakimbiza vizuri Waganda, alifanya makosa kama ya Kiemba baada ya kushindwa kutikisa nyavu dakika ya 20 kufuatia pasi ya Bocco, ambaye naye dakika moja kabla alikosa bao la wazi.
Taifa Stars waliendelea kuwanyong’onyesha mashabiki wake baada ya kushindwa kufunga kupitia kwa Bocco katika dakika 21 na 23, na baadaye dakika tatu Ngassa naye alikosa bao la wazi.
Shambulizi kubwa la The Cranes lilikuja dakika za 30 na 39, ambapo wangeweza kufunga mabao kama siyo nafasi hizo kupotezwa na Edema Patrick.
Pamoja na Kocha wa Stars, Kim Poulsen kusema bado kuna nafasi ya kushinda mchezo wa marudiano na kufuzu kwa michuano hiyo, matumaini ni kidogo.
Akitetea wachezaji wake kupata nafasi nyingi na kushindwa kufunga, Kim alisema: “Katika soka kukosa mabao ni jambo la kawaida, bado tunaweza kushinda kwenye mchezo wa marudiano.” Kocha wa Uganda, Sredojevic “Micho” Milutin alisema wachezaji wake walicheza kwa kujituma na ndiyo maana wakapata ushindi ugenini.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. taifa star ivunjwe ;
    TFF katafuteni vipaji KIGOMA

    ReplyDelete
  2. mnatuangusha washkaji.

    ReplyDelete

Top Post Ad