TFF KUIVUNJA TEAM YA TAIFA STARS

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema litaivunja Timu ya Taifa (Taifa Stars) mpaka Novemba mwaka 2014 iwapo itaondolewa na Uganda katika machi ya marudiano kusaka tiketi ya kucheza michuano ya CHAN mwakani.
Mwanza. Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Saad Kawemba amesema iwapo Timu ya Taifa (Taifa Stars) itafungwa katika mchezo wake wa marudiano dhidi ya Timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes), timu hiyo itavunjwa mpaka Novemba 2014.
Stars inahitaji ushindi wa mabao 2-0 ili kufuzu kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN). Katika mchezo wa kwanza Stars ililala bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa.
Akizungumza katika hafla ya mlo wa jioni iliyoandaliwa na Kampuni ya Bia ya Tanzania (TBL) juzi, Kawemba alisema hakutakuwa na sababu ya kuwa na timu ambayo haishiriki mashindano makubwa ya kimataifa, hivyo amewataka wachezaji kuhakikisha wanashinda mchezo wa marudiano.
“Sababu ya kuja kuweka kambi Mwanza ni kuhakikisha tunashinda mchezo wetu wa marudiano dhidi ya Uganda. Mwaka jana timu ilipoweka kambi hapa Mwanza, ilikwenda Kampala na kushinda mechi tatu kwenye michuano ya Chalenji iliyofanyika Uganda,” alisema Kawemba.
“Tupo Mwanza kwa sababu tunakwenda kucheza Kampala Julai 27, mwaka jana wakati wa Chalenji tuliweka kambi hapa na tulipotoka tulifika Kampala na kushinda mechi tatu mfululizo, sasa kama tupo Mwanza tena ni kwa nini tusiende kushinda mechi hii.”
Kawemba alisema ni jukumu la wachezaji kuhakikisha wanashinda mchezo huo ili kupata fursa ya kushiriki mashindano makubwa Afrika mwakani.
“Naamini timu yetu nzuri na inaweza kushinda mechi ya marudiano. Wachezaji hampaswi kuvunjika moyo na mashabiki kwa kufungwa mchezo wa kwanza. Mashabiki siku zote wanataka ushindi na siyo kufungwa,” alisema zaidi.
“Mashabiki ni watu wa kulaumu sana, wanataka timu ifanye vizuri na matokeo yanapokuwa kinyume chake wanakasirika,” alisema Kawemba na kuongeza:
“Wametusema viongozi kwamba tumeisahau timu na kuweka mkazo zaidi kwenye uchaguzi wa TFF. Hakuna ukweli kwenye jambo hili, TFF imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha timu inafanya vizuri kwenye mashindano.”
Kwa upande wake Meneja wa Kanda wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Malaki Sitaki alisema wadhamini hujisikia raha timu inapofanya vizuri kwenye mashindano.
“Imani yetu ni kuwa tunayo timu bora, nzuri na mategemeo yetu ni kushinda hata kwao. Kama walitufunga nyumbani, kwa nini na sisi tusiwafunge kwao?” alihoji Sitaki.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad