"TUTAKUCHAKAZA WEWE KAGAME NA RWANDA YOTE KAMA UKITHUBUTU KUTUCHOKOZA".....TANZANIA YAMJIBU RAIS KAGAME

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

SERIKALI ya Tanzania imeipa onyo kali nchi ya Rwanda ikiitaka isijaribu kuota ndoto za kuishambulia kijeshi, vinginevyo itajibu mapigo kwa nguvu zote na kuhakikisha kuwa imeichakaza.


Kauli hiyo ya kwanza nzito imetolewa jana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Kimataifa kufuatia taarifa ya matamshi makali yanayodaiwa kutolewa na Rais Paul Kagame wa Rwanda, dhidi ya Rais Jakaya Kikwete na kutishia kuishambulia Tanzania.


Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa wizara hiyo, Mkumbwa Ally, alisema ingawa Serikali ya Tanzania hadi sasa inajua haina ugomvi wowote na Rwanda, lakini amekiri kuwapo kwa kile alichokiita ‘kupishana lugha’ kwa Rais Jakaya Kikwete na Paul Kagame.


Mkumbwa alikiri Serikali ya Tanzania kunasa matamshi yanayodaiwa kutolewa na Rais Kagame katika moja ya hotuba zake aliyoitoa Juni 30, nchini kwake wakati akihutubia katika hafla moja ya vijana.


Kwa mujibu wa hotuba hiyo, ambayo kwa wiki sasa imesambazwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii, Kagame anadaiwa kusikika akitoa matamshi ya vitisho dhidi ya Rais Kikwete, kwamba anamsubiri katika wakati aujuao na kumchapa.


Baadhi ya maneno yanayodaiwa Rais Kagame aliwaambia vijana waliokutana katika mkutano wao uliojulikana kama ‘Youth Konnect’ na kufadhiliwa na mke wake, Janet Kagame, yanasema: “Huyu mtu mliyemsikia akiwa upande wa Interahamwe na FDLR na akashauri majadiliano….majadiliano?”


Aidha, Kagame anadaiwa kusema kuwa hatakuwa tayari kujadili jambo hilo, isipokuwa atamsubiri Rais Kikwete sehemu muafaka na ‘kumtandika’.

“Sitapoteza muda wangu kumjibu Kikwete, inajulikana maana kuna mahali hataweza kuvuka…haiwezekani,” alikaririwa akisema Rais Kagame, akilenga kumtisha Rais Kikwete.


Mbali na Kagame, baadhi ya viongozi kadhaa wa serikali ya Rwanda wamekuwa wakimshambulia Rais Kikwete wakimpachika majina ya kejeli ya; “Rais mhurumia magaidi, wauaji wa kimbari, mkorofi na mwenye dharau.”


Mkumbwa hata hivyo alisema Serikali ya Tanzania haina sababu ya kuingia katika vita na Rwanda, kwa sababu tu ya ushauri alioutoa Rais Kikwete wa kuitaka ikutane na wapinzani wake wanaoishi ndani ya nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kujadiliana kuhusu amani ya nchi za Maziwa Makuu.


Alisema msimamo wa Tanzania utabaki kuwa uleule wa kuitaka nchi hiyo ikubali kukaa meza moja na wapinzani wake, ili kumaliza migogoro inayoendelea katika nchi hizo za maziwa makuu, ambao unaungwa mkono na jumuiya ya kimataifa na SADC.

“Unajua mgogoro wa DRC na Rwanda hauwezi kumalizika bila ya nchi hizo kukaa meza moja na wapinzani wao ili kupata suluhu ya kudumu,” alisema Mkumbwa.


Aliwataka Watanzania kuwa watulivu na kuendelea na kazi zao kama kawaida, kwani serikali yao iko makini katika kulinda mipaka yake.

Chanzo cha mzozo
Msuguano baina ya nchi hizi mbili ulianza siku chache tu baada ya kumalizika kwa kikao cha viongozi wa nchi za Maziwa Makuu na ambacho kilihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, chini ya uenyekiti wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.

Rais Kikwete wakati akimtaarifu Rais Museveni kile walichokuwa wamekijadili katika kikao hicho kwa vile aliketi kwa muda kwa kuwa alichelewa kuwasili, alisema ni vema serikali za Rwanda na Uganda zifungue mlango wa mazungumzo na waasi wao na akaanza kutaja majina ya vikundi vya uasi vya nchi hiyo vilivyopo nchini DRC.

Habari zinasema kauli ya Rais Kikwete iliungwa mkono na Rais Museveni akisema: “Bila mazungumzo hatutafika popote pale”.  


Hata hivyo, matamshi hayo yalijibiwa kwa ukali na serikali ya Rwanda, kiasi cha kumlazimu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, kutoa tamko bungeni.


Kwa kauli yake, Membe alisema serikali ilikuwa imeshangazwa na shutuma hizo za Rwanda kwani halikuwa jambo baya kutoa ushauri uliolenga kuleta mapatano na kuepusha umwagaji zaidi wa damu wa wananchi. 

Akaongeza kuwa, ilikuwa ni wajibu wa Serikali ya Rwanda kuupokea ama kuukataa, na wala si kutoa maneno ya kejeli na vitisho.

Kauli ya Zitto
Akizungumzia kauli hiyo ya vitisho, mwanasiasa machachari hapa nchini na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, alisema ushauri wa Rais Kikwete kwa Rwanda ulikuwa wa busara mno na akashangaa kuona nchi hiyo jirani ikitoa vitisho, kejeli, dharau na ukosefu wa adabu kwa Kikwete.
 
Katika moja ya tamshi lake alilolitoa jana katika mitandano ya kijamii, Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA) alisema Marekani wanaongea na waasi wa kundi la Taliban, hivyo hakuna dhambi kwa Rwanda pia kufanya hivyo.

“Pia kama hutaki ushauri si unakataa tu, sasa kuanza kurushiana maneno ya nini tena? Hutaki ushauri basi. 

Maneno ya kila siku ya nini? Tangu Kikwete amesema kule Addis, hajasema tena. Membe (waziri) akajibu Dodoma Tanzania haijasema tena. Kigali inasema mambo haya kila siku kwa ajili ya nini?


Taliban na Al Qaeda si wale wale? Wale watoto waliozaliwa mwaka 1994 na wakimbizi wa Kihutu waliopo Kongo nao ni wauaji? Tufikiri vizuri mambo haya. Kuna ‘genociders’ wasakwe, wakamatwe wahukumiwe. Kuna watu wana haki kabisa ya kutaka kushiriki kwenye siasa za Rwanda na wanazuiwa, wameshika silaha. Hawa lazima wakae meza moja wakubaliane,” alisema Zitto.

Mwanasiasa huyu alisema kwa sasa serikali za nchi hizo mbili zinatakiwa kuingia katika vita ya kupambana na kuondoa umasikini wa watu wake na si vita ya mtutu wa bunduki.

Busara itumike kwa viongozi ‘neutral’ kama Uhuru Kenyatta kuwaweka pamoja Kagame na Kikwete wamalize tofauti zao. Haya maneno hayana maana yoyote,” alisema.

Alisema vita haitamuumiza Rais Kagame wala Rais Kikwete na familia zao, bali itaumiza wananchi wa kawaida wa mikoa ya Kagera na Kigoma na mikoa ya mpakani ya Rwanda.


Vita itaturudisha nyuma sana kwenye juhudi za maendeleo. Vita itazima harakati za kujenga demokrasia nchini.  Busara itumike tu,” alisema Zitto.

Tanzania Daima
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

17 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kikwete anazuga tu na kujaribu bila mafanikio kuhamisha mjadala wa kitaifa na hali mbaya ya amani aliyoivuruga hapa tanzania kwa mikono yake mwenyewe inayonuka damu.Utaweza je kumshauri Kagame kabla ya kutatua matatizo ya tanzania ambako polisi,ccm na usalama wa taifa wanateka,kutesa,kung'oa meno,kunyofoa kucha na kuua raia? Kikwete anapenda sana political musterbation!

    ReplyDelete
  2. Kikwete ni kama demu tu kwa kidume rijali Kagame.Kagame ,usiache kumpiga miti kikwete akiingia kwenye kumi na nane zako!

    ReplyDelete
    Replies
    1. ANONYMOUS KIKWETE NI KAMA DEMU WEWE MWENYEWE NI DEMU SIO KAMA SO ACHA UJINGA WEWE MBULULA WA FIKRA FISI MAJI.

      Delete
  3. inchi ya siasa kali baba tanzania inaitwa chokoza ukawone. mtakipata cha mtemakuni

    ReplyDelete
  4. Big-up Kikwete nashangaa hawa mang'ombe wanaokuponda wakati wao hawawezi kuteuliwa hata kuwa balozi wa nyumba kumi, watabaki domo tu but nothing they know

    ReplyDelete
  5. vita haina faida,tusubli tuchokozwe mkuu,pili mtu mpumbavu mlekebishe bla ugonv,naye atakushukulu

    ReplyDelete
  6. Kwanini tunagishukuu? Kagame hajamtajaa mtuu...amesema about those one who surpport interahamwee Atapambana nao...is Kikwete among them?? If he is not among them,why do you have borther?? Si Rais wetu hausiki na nterahamwe...then why are we shauting at Kagame?

    ReplyDelete
  7. Kwanini tunagishukuu? Kagame hajamtajaa mtuu...amesema about those one who surpport interahamwee Atapambana nao...is Kikwete among them?? If he is not among them,why do you have borther?? Si Rais wetu hausiki na nterahamwe...then why are we shauting at Kagame?

    ReplyDelete
  8. Kwanini tunagishukuu? Kagame hajamtajaa mtuu...amesema about those one who surpport interahamwee Atapambana nao...is Kikwete among them?? If he is not among them,why do you have borther?? Si Rais wetu hausiki na nterahamwe...then why are we shauting at Kagame?

    ReplyDelete
  9. Kwanini tunagishukuu? Kagame hajamtajaa mtuu...amesema about those one who surpport interahamwee Atapambana nao...is Kikwete among them?? If he is not among them,why do you have borther?? Si Rais wetu hausiki na nterahamwe...then why are we shauting at Kagame?

    ReplyDelete
  10. Kwanini tunagishukuu? Kagame hajamtajaa mtuu...amesema about those one who surpport interahamwee Atapambana nao...is Kikwete among them?? If he is not among them,why do you have borther?? Si Rais wetu hausiki na nterahamwe...then why are we shauting at Kagame?

    ReplyDelete
  11. kagame akiyakanyaga anyooshwe tu, tumeshachoka mikwara, vijinch vdg vdg kama mikoa, pambafuuuuuuuuu........!

    ReplyDelete
  12. Try Kagame and see the secret in his small country of his....God can't give big country and the power.mbinu za vita vip??? au ni makelele tuu?

    ReplyDelete
  13. Try Kagame and see the secret in his small country of his....God can't give big country and the power.mbinu za vita vip??? au ni makelele tuu?

    ReplyDelete
  14. Try Kagame and see the secret in his small country of his....God can't give big country and the power.mbinu za vita vip??? au ni makelele tuu?

    ReplyDelete
  15. daniel yona sumari15 July 2013 at 12:45

    Nyie mmbwa mnao mponda raisi kikwete wekeni maslai ya taifa mbele nasio kubeza kila chenye mafanikio. Nyie mlitaka raisi wa nchi hii awe baba yenu?msilete siasa kwenye jambo hili.

    ReplyDelete
  16. For the sake of the citizens of both countries ,Kagame and Kikwete they won't fight and they will never fight ok. Brothers don't fight they just get miss understings! Who will allow them to fight???? Lukuusa kawapaaa nani??? Ebu ingueni DRC mkaibe madini ni mengi sanaaa bado.

    ReplyDelete

Top Post Ad