WACHEZAJI TAIFA STARS WADAIWA KUTOJITUMA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kampala. Imeelezwa kuwa changamoto kubwa inayoikabili Timu ya Taifa (Taifa Stars) kiasi cha kudhoofisha mipango yake ya kusaka mafanikio ni baadhi ya wachezaji wanaoitwa kuitumikia kukosa uzalendo kwa nchi yao.
Habari za ndani ilizozipata Mwananchi zinadai kuwa, Kocha wa Stars Kim Poulsen amekuwa akikutana na wakati mgumu katika kazi yake kwani baadhi ya wachezaji wamekuwa wakigoma kujiunga na timu hiyo pale wanapoitwa.
Hali hiyo imedaiwa kuwa chanzo cha mafaniko duni ya kikosi hicho, kwa vile baadhi ya wachezaji wamekuwa hawajitumi uwanjani.
Chanzo hicho kilisema kuwa, Kim alilazimika kufanya kazi ya ziada kuwashawishi baadhi ya wachezaji tegemeo kujiunga na kikosi chake kwa ajili pambano dhidi ya Uganda lililopigwa jana kwenye Uwanja wa Mandela jijini Kampala.
“Tunafanya jitihada za dhati ili Tanzania iweze kufikia mafanikio lakini kuna vikwazo tunakutana navyo kama baadhi ya wachezaji kukosa uzalendo,” kilidai chanzo hicho na kuongeza:
“Mfano John Bocco na Sure Boy (Abubakar Salum) hawakutaka kwenda Mwanza ilimbidi Kim na Marsh (kocha msaidizi wa Stars) wafanye kazi ya ziada kuwashawishi ndiyo wakakubali,”.
Mbali ya Bocco na Sure Boy, mchezaji mwingine ambaye alitaka kujiondoa kwenye kikosi chake kwa madai kwamba hathaminiwi kutokana na kutopangwa katika mechi kuwa Athuman Iddi.
“Unajua Chuji huwa anaitwa lakini hatumiwi na Poulsen Stars hivyo akasema anajitoa kwa sababu umuhimu wake hauonekani, lakini kukosekana kwa Mwinyi Kazimoto kukamfanya Kim amshawishi aendelee kuwapo kikosi,” kilisema chanzo hicho.
Pia ilidaiwa kuwa hata wakati kikosi cha Stars kilipokuwa jijini Mwanza, Boko na Sure Boy walitaka kugoma kwenda Kampala, ambapo Poulsen na Marsh walipochukua jukumu la kuwashawishi na ndipo wakakubali upanda ndege.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad