AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Tukio hilo lilijiri mahakamani hapo Agosti 22, mwaka huu ambapo mshitakiwa alikana mashitaka mbele ya Hakimu Mfawidhi, Joyce Minde.
Trafiki feki huyo alitumia muda mwingi kujificha sura ili kamera zisimchukue lakini alichemsha kwani kila alipojifunua kidogo alikuta kamera ziko mbele yake.
Hali hiyo ilimfanya mshitakiwa huyo aamue kujiachia kwa kutoa kofia aina ya kapelo kichwani na picha za kumwaga kupatikana.
Akisoma mashitaka hayo, Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Nassoro Katuga alisema mnamo Agosti 14, 2013, huko Tabata Kinyerezi Mnara wa Voda, Dar, mtuhumiwa alikutwa amevaa nguo za askari wa usalama barabarani akijifanya ni mwajiriwa wa jeshi la polisi jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Hata hivyo, mshitakiwa alipelekwa rumande Segerea, hadi Septemba 5, 2013 baada ya kukosa wadhamini wawili kwa shilingi milioni kumi na nne.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
maskini alikuwa anatafuta tu maisha nayeye maskin mngemuachia tuu dii
ReplyDelete