VITUO VYA MWENGE NA UBUNGO KUHAMISHWA JIJINI DAR

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Vituo vya daladala vya Ubungo na Mwenge vinahamishwa kupisha Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka Dar es Salaam (DART), ambao miundombinu yake inaendelea kujengwa.

Ofisa Habari wa Manispaa ya Kinondoni, Sebastian Mhowera amekaririwa akisema yafuatayo:-
Kituo cha Ubungo kitahamishiwa nyuma ya jengo la Mawasiliano lililopo Barabara ya Sam Nujoma.
Kituo cha Mwenge, kitatumika kwa ajili ya kushusha abiria pekee.
Magari ya Mwenge, yatakuwa na uamuzi wa ama kuishia kwenye stendi ya Makumbusho au kwenda hadi kituo hicho kitakachohudumia magari ya Ubungo (kilichoko Mawasiliano).
Wakati wowote kuanzia sasa vituo hivyo, vitabomolewa kupisha mradi huo.

Kuhusu hatua zinazochukuliwa na manispaa, kuwezesha wafanyabiashara ndogo kupata maeneo ya kuendesha shughuli zao alisema, hakutakuwa na mfanyabiashara atakayeruhusiwa kuuza bidhaa zozote katika kituo kipya, kama ilivyo sasa kwa vile hakutakuwa na nafasi kutokana na  eneo lote kutumika kwa ajili ya barabara.

Akasema kwa hali hiyo wafanyabiashara watalazimika kwenda katika maeneo waliyopangiwa: “ Kwa hiyo ni bora wakaanza kujiondosha wenyewe mapema kabla hatua ya kuondolewa na ujenzi kuwafikia,” alisema na kuongeza kuwa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kazi hiyo yapo katika masoko mbalimbali likiwemo la Kijitonyama.


Habari leo

Udaku Specially Blog
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hiya! Quick question that's totally off topic.
    Do you know how to make your site mobile friendly? My website
    looks weird when browsing from my iphone4. I'm trying to find a template or plugin that might be able to correct this issue.
    If you have any recommendations, please share. With thanks!
    Quest Bars blogesaurus

    ReplyDelete

Top Post Ad