CCM "SISI TUNA IMANI KUBWA NA TUME YA KATIBA"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa msimamo wake kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya unaoendelea nchini kikieleza kuwa kinaiamini na kuiheshimu Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Jaji mstaafu Joseph Warioba ambaye ni mwenyekiti.

Kauli hiyo ya CCM imekuja kipindi ambacho Jaji Joseph Warioba akivishutumu vyama vya siasa kuingilia mchakato huo, huku akivionya kwamba  mapendekezo yaliyomo katika Rasimu ya Katiba yametoka kwa wananchi, siyo vyama vya siasa.

Ufafanuzi huo wa CCM unaonekana kama kutaka kuweka mambo sawa baada ya hivi karibuni vyombo vya habari kumnukuu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya chama hicho, Abdallah Bulembo akisema siyo sahihi kwa Jaji Warioba kuwa msemaji wa Watanzania kuhusu mambo wanayoyataka yaingizwe ndani ya Katiba.

Katika majibu yake, Jaji Warioba alimtaka  Bulembo kuacha kupiga kelele dhidi yake kwa maelezo kuwa hakumtuma kazi ya kukusanya maoni ya Katiba Mpya, bali alitumwa na Serikali kwa niaba ya wananchi

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi Ndogo ya CCM  Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye alisema kuwa chama hicho tawala kinaiheshimu tume hiyo na kamwe hakiwezi kuiingilia.

Nape alisema tume hiyo iliteuliwa kwa ajili ya kukusanya maoni ya wananchi kuhusu Katiba Mpya, hivyo wanaiheshimu na wana imani nayo. “Tunaheshimu tume, tuna imani nayo na tunaahidi ushirikiano wa kutosha katika mchakato wa Katiba" alisema Nape.


Kauli ya Nape imekuja wakati ambao kuna msuguano kati ya CCM na Serikali yake kwa upande mmoja na vyama vitatu vya upinzani vyenye wabunge ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Udaku Specially Blog
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad