AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na Mtandao huu, kiongozi wa Mtanashati Entertainment Ustaadh Juma Namusoma alisema kuwa sababu za kumtimua Dogo Janja ni utovu wa nidhamu, unywaji pombe, kutokwenda shule pamoja na uvutaji bangi.
Aliongeza kuwa tayari amempatia nauli ya basi shilingi 90,000/= kurudi nyumbani kwao jijini Arusha alipotokea. Dogo Janja alitua kwa mbwembwe jijini Dar es Salaam kwa ndege Juni 22 mwaka jana akitokea Arusha na kujiunga na kundi hilo.
Awali alikuwa katika kundi la Tip Top Connection linaloongozwa na Madee lakini ilitokea kutoelewana kati yao na kurudishwa kwao Arusha. Alipopigiwa simu na Mtandao huu, Dongo Janja alidai kuwa bado ni memba hai wa Mtanashati Entertainment.
-GPL
Udaku Specially Blog
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Ndo atatia akili
ReplyDeleteUjanja wote utamtoka
ReplyDeleteMakundi ya watu wazima ndo yaamharibu huyu dogo...Tunda la msimu
ReplyDeleteatulize akili
ReplyDeleteyaan mtt mdogo ndiyo yaleyale ya kina lulu badala wasome wanaanza mambo ya ukubwa wangali bado watt. matokeo yake wanapoteza kabisa muelekeo
ReplyDelete