MWANZA: WAJAWAZITO WANYWESHWA MAJI YA MBWA ALIYEJIFUNGUA PAMOJA JASHO LA WAUME ZAO ILI KUONDOA MIKOSI

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Imani za kimila wilayani Misungwi mkoani Mwanza zinadaiwa kusababisha baadhi ya wajawazito kunyweshwa maji machafu yakiwemo yaliyofuliwa shati la mume husika anayetuhumiwa kufanya ngono wakati mke akiwa mjamzito, kwa kile kinachodaiwa ni kuondoa mkosi ili mjamzito husika ajifungue salama.

Katika jamii ya wenyeji wilayani hapa, ni kwamba mjamzito anaposhiriki katika tendo la ndoa na wanaume wengi, hupata kifafa cha mimba siku ya kujifungua na dawa yake ni kunyweshwa maji yaliyolowekwa mchanga kutoka eneo alilowahi kuzalia mbwa.

Hayo yalielezwa katika mafunzo ya afya yanayoendelea wilayani hapa. Kuhusu kunyweshwa maji yaliyofulia shati, Mhudumu wa Afya katika Kijiji cha Mwamanga, Manyanda Kanyumbo alisema ikitokea mjamzito akachelewa kujifungua na ikagundulika mumewe alikuwa na uhusiano na wake wengi, shati lake hufuliwa na kisha mjamzito huyo hunyweshwa maji yaliyotumika.

“Watu wanaamini akishakunywa maji machafu ya mumewe hujifungua haraka na salama na kikombe alichonywea hufunikwa uvunguni mwa kitanda hadi atakapojifungua”, alisema.

Kwa upande wa mjamzito aliyetembea na wanaume wengi, jamii inaamini kwamba ili aweze kujifungua salama, lazima uchukuliwe mchanga sehemu ambayo mbwa amewahi kuzalia, ulowekwe kwenye maji na kisha mjamzito husika anywe kuondoa mkosi kabla ya siku ya Katika mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na hospitali ya Aga Khan kwa kushirikiana na Chuo cha Maendeleo na Ushirika cha MS TCDC kilichoko jijini Arusha, Kanyumbo alisema, “wanaamini kabisa mwanamke ambaye amechangia wanaume wengi, siku ya kujifungua kuna uwezekano mkubwa wa kupata kifafa cha mimba”.

Kanyumbo aliendelea kusema, “ili aweze kujifungua salama, bibi hufuata mchanga wa sehemu aliyozalia mbwa na kuuloweka kisha humnywesha, maana tunaamini mbwa hukutana na mbwa wengi ili aweze kutunga mimba, wale mbwa wengi huwafananisha na wanaume wengi.”

Jacqueline Martin muuguzi wa Mwanangwa, alisema baadhi ya watu wanaamini mjamzito akivuka mto, mtoto wake hazaliwi mapema na pia mwanamke huyo haruhusiwi kunywa maji akiwa amesimama.

Wanadai akinywa maji akiwa amesimama siku ya kujifungua, mtoto hawezi kushuka haraka.

Vile vile wanaamini mjamzito akikaa kwenye jiwe au kinu, mtoto huchelewa kuzaliwa. --- via HariLeo
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

5 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mh! Uchafu ajabu

    ReplyDelete
  2. mila nyengine uchafu tu!

    ReplyDelete
  3. MMLIKI WA HII BLOG NA BLOGGERS WENGINE, EBU ACHEN TABIA MBAYA YA COPY AND PEST, HABARI MOJA IKO BLOG ZAIDI YA 20, NA HII NIMEISEMA HATA KWA BLOG NYINIGNR NAJUA HAWATAIRUSHA, ACHEN HIZO, MSIPENDE HELA YA MTEREMKO, TAFUTEN HABAR NA LETEN WATU TUSOME, NDIO MAANA MANGE ANAKUWA JUU, WATU WANAKALIA TU KUMCHIKIA, SABABU YEYE MAMBO YA COPY NA PEST NI MWIKO HATA AKIFANYA KWA HABAR CHACHE UTAFURAHI MWEYEWE, KUWEN WABUNIFU.UMELALA TU NYUMBANI NA KUANZA KUAPLOAD HABARI KUTOKA KWA WENEZENU WALIOFANYA KAZI, TENA HASA MNAONGOZA KWA KUCHUKUA HABAR GLOBAL PUBLISHERS, ACHEN HIZO, ASIYEFANYA KAZI NA ASILE.manapata UMAARUFU kwa habar za wenzenu.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Alafu hii habari hata haujasema source yake

      Delete
  4. hiyo ni hatari sana

    ReplyDelete

Top Post Ad