Rihanna amejikuta kikaangoni tena wiki hii baada ya mashabiki wake kumshambulia kutokana na video yake mpya ya wimbo ‘Pour It Up’ wakisema ni chafu na ina matusi mno. Mamia walitumia mitandao ya kijamii kumponda mrembo huyo kwamba ‘hana hata haya’ kutoa video chafu kama hiyo.