google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html SIMBA NA YANGA PRESHA TUPU...KOSA MOJA TU KWISNEY | UDAKU SPECIAL

SIMBA NA YANGA PRESHA TUPU...KOSA MOJA TU KWISNEY

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Vinara wa Ligi Kuu, Simba wanafahamu  kwamba, watani zao Yanga wanawasubili kwa hamu wafanye makosa tu wawashushe kileleni.

Simba leo watashuka kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwakaribi Tanzania Prisons kwa lengo moja tu la kupata ushindi ili kuendelea kubaki kileleni.

Mahasimu wao wakuu, Yanga ambao pia leo watateremka Uwanja wa Kaitaba mjini  Bukoba kumenyana na Kagera Sugar, wapo katika nafasi ya nne na pointi zao 12.

Hiyo ina maana kwamba kama Simba itavuna pointi tatu au sare itaendelea kukaa kileleni, lakini kama itapoteza na Yanga kushinda na kufikisha pointi 15 itakuwa imekiweka rehani kiti chake cha uongozi, kwa vile hatima hatma yao itaamuliwa na kigezo cha uwingi wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Pia, Simba inafahamu madhara ya kupoteza mchezo huo hasa baada ya kusakamwa kwa karibu na Azam FC na Mbeya City ambazo kila moja imejikusanyia pointi 14 na kama zitashinda mechi zao zijazo zitakuwa na fursa ya kukaa kileleni.

Kocha wa Simba Abdalah Kibadeni ‘King’ alisema: “ Tupo tayari kwa ajili ya kuikabili Prisons, kwa vyovyote vile mchezo utakuwa na ushindani mkubwa lakini tumejiandaa kwa ajili ya kuhakikisha tunaibuka washindi.”.

Naye Kkocha wa Yanga,Ernest Brandts alisema: “Wachezaji wangu wote wapo katika hali nzuri wakiwa na morali kubwa ya kuhakikisha wanashinda.” Kwa upande wake, Kocha wa Prisons, Jumanne Chale alisema: “Simba ni timu ya kawaida kama zilivyo timu zingine,

hatuihofii wala kuigopa, baada ya dakika tisini nina uhakika matokeo mazuri yatakuwa upande wetu”.


Kocha Msaidizi wa Kagera, Mlage Kabange alisema: “Nadhani hakuna namna ambayo Yanga wataepuka kipigo, vijana wangu wamepania kuendeleza ubabe kama ilivyoku wenye Uwanja wa Azam Complex vibonde wa ligi hiyo, Ashanti United wataivaa Coas tal Union.

Udaku Specially Blog
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad