ASKOFU BILIONEA ATIKISA BONGO

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Stori: Jelard Lucas
ASKOFU na Nabii George David ‘Geordavie’ wa Kanisa la Geordavie Ministry ‘Ngurumo ya Upako’ lililoko jijini Arusha na Kawe, Dar hivi karibuni alifanya mkutano mkubwa na kutikisa nchi  kwa kuwa na magari ya kifahari na ndege aina ya helikopta ‘chopa’ iliyokuwa ikirandaranda juu ya anga kulinda usalama wake, Uwazi lina ushuhuda wa kutosha.

Katika mkutano huo uliofanyika Karatu mkoani Manyara, mwandishi wetu alishuhudia msafara wa Geordavie ambaye hutoa huduma ya uponyaji kwa njia za miujiza, ukiwavutia watu wengi kwa kuwa ulikuwa na ulinzi mkali ambao haujawahi kutokea.

Mbali ya kuwa na chopa iliyokuwa ikiimarisha ulinzi ambayo ameinunua hivi karibuni, askofu huyo alikuwa na msururu wa magari yenye thamani kubwa yanayomfanya kutajwa kuwa tajiri kuliko maaskofu wengine wanatoa huduma katika makanisa ya kiroho Tanzania.

Akiwa Karatu, mbali na ulinzi binafsi, Geordavie alikuwa akilindwa na askari wa jeshi la polisi, askari kanzu, Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) na wale wa usalama barabarani.

Mbali na askari hao wa serikali ambao wamekuwa wakimlinda kila anapofanya mikutano yake, pia Geordavie analindwa na askari wake binafsi hali iliyowafanya baadhi ya watu kuamini kuwa ulinzi wake ni kama ule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’.

“Sijawahi kumuona JK akilindwa na chopa lakini mtumishi wa Mungu Geordavie analindwa na ndege katika msafara wake! Hii ni mara yangu ya kwanza kuona,” alisema muumini mmoja ambaye hakupenda kutajwa gazetini.

Hata hivyo, baadhi ya watu walikuwa wakihoji utajiri wa askofu huyo kutokana na fedha nyingi anazozitumia anapofanya mikutano katika sehemu mbalimbali jijini Arusha.

“Tunajua kuwa ni tajiri, lakini anapata wapi fedha za kutumia hivi?” alihoji muumini aliyejitambulisha kwa jina moja la Julius ambaye naye alihudhuria mkutano wa askofu huyo anayetumia kaulimbiu ya Ngurumo ya Upako katika kutoa huduma yake.

Pia, waumini wengine walilalamikia ugumu wanaoupata wanapotaka  kumuona mtumishi huyo wa Mungu kutokana na ulinzi mkali anaopewa.

“Kila mtu alitamani kumuona mtumishi wa Mungu lakini haikuwezekana kutokana na ulinzi wake kuwa mkali, utajiri wake hakuna mfano, hata kule nyumbani kwake Arusha, anaishi kama Mfalme Daud,” alisema Fred Mushi.

Gazeti hili lilimsaka Askofu na Nabii Geordavie kwa lengo la kutaka kujua sababu ya kuwa na ulinzi mkali na kutumia magari ya kifahari ikiwemo chopa katika mikutano anayoifanya lakini simu yake iliita bila kupokelewa.
Credits:Global Publishers
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

13 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. chezea upako wa nigeria wewe

    ReplyDelete
  2. ......shit! this is devilish! Mtumishi wa Mungu hategemei ulinzi kwa wanadam! Bali aliye mtumishi kweli wa Mungu ulinzi wake hupewa na Mungu ambao ni ulinzi thabiti kuliko!!! Imani yake I haba hadi asiuamini ulinzi wa Mungu na kuweka walinzi watu? Tupo ktk nyakati za Mwisho tutegemee kuona makubwa zaidi ya hayo! Aonaye haitaji kuambiwa kwani imenenwa kuwa maarifa tumejaaliwa na Mwenyezimungu lakini twaangamia kwa kukosa kuyatumia maarifa hayo!!!!

    ReplyDelete
  3. Muacheni Dady wetu, utajiri wake haukuhusu wewe nyan'gau pita hiviiiii

    ReplyDelete
  4. Nani alisema mtumishi wa mungu hajilindi ?ulishajiuliza kuhusu ulinzi wa pope?unaijua garama inayotumika kumlinda na kwanini? Ujawahi ona au sikia viongozi wa dini wanafanyiwa maasi na waumini feki?mungu alisema JISAIDIE NDIPO NA YEYE AKUSAIDIE.

    ReplyDelete
  5. Hayaaaaaaaaaaa! Yetu macho watu mwogopeni mungu sana , manabii wengi BONGO wanatumia nguvu za giza na binadamu tumesoma sana vitabu vya DINI lkn atuogopi kabisa ushetani tu umewazunguka ( yehova tulinde kwa hili Ghalika Amen)

    ReplyDelete
  6. Ishara zote ndo zinazidi kutimia.

    ReplyDelete
  7. Jamani biblia imesema shikeni mlichonacho, siku za mwisho watakuja manabii wa uongo, ndo hawa, mashetani wanajifanya manabii, toka lini nabii akajiamulia yeye ni nabii, mshindwe kwa jina la Yesu, jehanam inawasubiri.

    ReplyDelete
  8. Jamani nisali kanisa lipi?haya mambo hata bila kuambiwa utang'mua kwamba ni nguvu za Giza ,ushetani mtupu na u freemason.

    ReplyDelete
  9. KWANI HAMJUI SIKU HIZI MAKANISA MENGI UAMEGEUZWA NI SACOSS ZA KUKUSANYA PESA ZA WAPUMBAVU??ACHA ALE MAISHA .SI UJINGA WENU WENYEWE NA MNAMPELEKEA SADAKA WENYEWE??SASA MNASHANGAA NINI?

    ReplyDelete
  10. acheni kuongelea ya watu wakati hamjui chochote. eti asijilindi kwani nyie hamuoni viongozi wakubwa wadini na wanajilinda.

    ReplyDelete
  11. muuza senbe tuu huyu

    ReplyDelete

Top Post Ad