google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html MCHEZAJI WA YANGA WA ZAMANI ANYONGWA DAR | UDAKU SPECIAL

MCHEZAJI WA YANGA WA ZAMANI ANYONGWA DAR

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

OMAR Changa, straika aliyekuwa na umbo la mwili lililokuwa likiendana na nafasi yake hatunaye, na habari kutoka kwa ndugu zake zinasema alinyongwa na watu wasiojulikana pamoja na kuchomwa na kitu chenye ncha kali maeneo ya kichwani na ubavuni.

Mchezaji huyo aliyetamba na Yanga alizikwa jana Jumatatu jioni katika makaburi ya Mwinyimkuu, Magomeni Dar es Salaam huku kifo chake kikiacha maswali mengi ya utata kuliko majibu.

Kwa mujibu wa kaka wa Changa, ambaye alikuwa mchezaji wa Moro United iliyoshuka daraja, kaka wa marehemu Idd Kambi, ameliambiaa Mwanaspoti kuwa kwa mujibu wa ripoti ya daktari aliyokabidhiwa baba wa marehemu, inaonyesha kuwa Omar Changa alichomwa na kitu chenye ncha kali mgongoni na kilichotokeza mbele ye tumbo huku pia shingo ikionekana kulegea.

“Mpaka sasa tumemaliza mazishi, lakini bado tuna huzuni kuhusu hii ripoti tuliyopewa, tunachofanya tunafuatilia ni timu gani aliichezea mara ya mwisho kwa sababu inaonekana inafichwa, lengo ni kujua mazingira ya mchezo yalikuwaje.”

Mdogo huyo wa marehemu alisema Omar Changa alimpigia simu Jumamosi iliyopita, akimtaka kwenda naye kushuhudia anavyocheza ndondo mchangani maeneo ya Kigamboni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Katika mchezo huo Changa alifunga bao moja la ushindi kwa penalti.

Mchumba wake marehemu aliyetambulika kwa jina la Sarah Mahemba alisema Changa hakurudi kwake tangu alipoondoka Jumamosi kuelekea Kigamboni katika mchezo huo, jambo ambalo liliwapa shaka wapangaji wenzake siku ya Jumapili na kuamua kumtafuta kupitia simu yake ya mkononi lakini haikupatikana ingawa yeye aliijaribu na kuwa inaita bila kupokelewa mpaka alipopata taarifa za kifo kupitia mdogo wa mshambuliaji wa Mbeya City, Omari Kijuso.

Mwili wa marehemu ulipatikana katika mtaro, maeneo ya Jangwani jijini Dar es Salaam.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad