NI MARUFUKU KUVAA VIMINI BUNGE LA KATIBA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Dodoma. Wajumbe wanawake wa Bunge Maalumu la Katiba na wageni wa jinsi hiyo watakaovaa nguo fupi ‘vimini’ au nguo za kubana, hawataruhusiwa kuingia ndani ya Ukumbi wa Bunge.

Hayo yamo katika mapendekezo ya rasimu ya kanuni za uendeshaji wa Bunge hilo, zilizowasilishwa katika semina mahsusi ya kupokea rasimu hizo, iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Kamati Maalumu, Profesa Costa Mahalu.

Kanuni ya 82 (9) ya mapendekezo hayo imeainisha vazi rasmi linaloruhusiwa kuwa ni vazi lolote la heshima ambalo siyo la kubana mwili, lisiloonyesha maungo.

Pia imeainisha mavazi yanayoruhusiwa kwa wanawake kuwa ni pamoja na gauni la kitenge au blauzi inayovaliwa na kitenge au sketi ya rangi yoyote, suti ya kike, vazi linalovaliwa wakati wa eda na kilemba cha kadri au mtandio.

Kwa upande wa wanaume, mavazi rasmi ni suti ya Kiafrika au safari ya mikono mirefu au mifupi yenye ukosi au shingo ya mviringo na fulana.

Kulingana na kanuni hiyo, upande wa wanaume, pia imeainisha vazi rasmi kwa jinsia hiyo kuwa ni suti ya Kimagharibi, shati na tai, suruali ya aina yoyote isipokuwa suruali aina ya ‘jeans’.

Sehemu ya 6 ya kanuni hiyo, imeweka wazi kuwa mjumbe yeyote wa Bunge Maalumu, anaweza kutoa taarifa kwenye Bunge au kwenye kamati iwapo mjumbe mwingine ataingia akiwa amevaa vazi linalovunja au kukiuka masharti ya kanuni.

“Mwenyekiti wa Bunge Maalum au mwenyekiti wa kamati maalumu atakaporidhika kuwa mjumbe huyo aliyetolewa taarifa hajavaa vazi rasmi, atamwamuru atoke nje ya ukumbi wa mikutano wa kamati,” inaseme sehemu ya kanuni hizo.

Kwa mujibu wa kanuni hiyo, mjumbe aliyeamriwa kutoka nje ya ukumbi, hataruhusiwa kuingia tena hadi pale atakapokwa amevaa mavazi rasmi.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. sasa jamani hivi kweli nao watashindwa kujiheshimu kama wataenda na vimini humo bungeni

    ReplyDelete
  2. Kweli na hao ni wa viuo vikuu hata wawekewe dressing code kweli sasa tutamwamini nani awe kioo cha mtazania

    ReplyDelete
  3. c ndo wanasema uzeee mwisho chalinze,

    ReplyDelete

Top Post Ad