ANGALIA PICHA NDEGE SITA ZILIZOWAHI KUPOTEA DUNIANI HIZI HAPA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

1. Amelia Earhart - 1937

Rubani wa Kimarekani, Amelia Earhart alikuwa mwanamke wa kwanza kuvuka Bahari ya Atlantic kuchunguza dunia, alipotea na ndege yake miongo saba iliyopita. Inahisiwa kuwa ndege yake iliishiwa mafuta na kuanguka. 
2. Airbus A330 - 2009
 Mwaka 2009 ndege ya Shirika la Ndege la Ufaransa, Airbus A330 iliyokuwa na abiria 228 ikitoka Rio de Janeiro, Brazil kwenda Paris, ilipotea kwa siku tano. Ilipatikana ikiwa imeanguka na kuungua. Hadi sasa maiti za abiria 74 bado hazijatambulika.

3. Flying Tiger 739 - 1962
 Mwaka 1962 ndege ya kijeshi ya Marekani ilipotea ikiwa na watu 90 waliokuwa wanakwenda Ufilipino. Rubani wa ndege hiyo hakuwahi kutoa taarifa yoyote ya dharura na hadi sasa haijaonekana licha ya wataalamu 1,300 kushiriki kuitafuta.
4. South American Airways - 1947
 Ilichukua miaka 50 kupata fununu za ndege ya Amerika ya Kusini iliyopotea mwaka 1947 ikiwa na abiria 11 na kupatikana mwaka 1998 katika Milima ya Andes. Ndege hiyo ilifunikwa kwenye barafu ya milima hiyo.
5. Bermuda Triangle - 1948 na 1949
 Ulikuwa ni mfuatano wa matukio ya kupotea kwa ndege mbili katika eneo la baharini linaloitwa Pembetatu ya Shetani (Devil’s Triangle) katika maeneo ya Florida, Puerto Rico na Bermuda ambalo limekuwa na matukio mengi ya kupotea kwa ndege na meli kimiujiza. Katika matukio hayo mawili, ndege hizo zikiwa na jumla ya abiria 51 zilipotea na hata wanaanga 13 waliotumwa kuitafuta pia walipotea.
6. Uruguay 571- 1972
 Ndege ya Shirika la Ndege la Uruguay, 571, ilipotea mwaka 1972 ikielekea Santiago, Chile. Ndege hiyo ambayo ilikuwa na abiria 45, ilianguka milimani na watu 12 walikufa. Walionusurika walitafutwa kwa zaidi ya siku 72. Kabla ya kuokolewa, majeruhi hao walilazimika kula nyama za wenzao waliokufa ili kuishi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kwa njia hii kwalarumpa wasikate tamaa waendelee kutafuta Mwenyezi MUNGU atawasaidia.

    ReplyDelete

Top Post Ad