DIRECTOR NICK DIZZO AACHANA NA E-MEDIA SASA AMEANZISHA KAMPUNI YAKE MWENYEWE INAITWA FOCUS FILMS

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kama umeshaiona video mpya ya rapper anaeiwakilisha Mbeya City, Izzo Bizness ‘Tummoghele’ iliyotoka rasmi Ijumaa iliyopita, utagundua kuwa video hiyo imefanywa na director yule yule aliyefanya video zake zilizopita aitwaye Nick Dizzo lakini safari hii sio kupitia kampuni ya E-Media

Nick Dizzo ameiambia Bongo5 exclusively kuwa kwa sasa ana kampuni yake mpya iitwayo ‘Focus Films’ ambayo imechukua nafasi ya E-Media aliyokuwa akishirikiana na Sama Jahn.

“E-Media pia ilikuwa company yangu, ila kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wangu kwa sasa natumia company yangu mpya ya Focus Films, ina team mpya ambayo iko focused zaidi kwenye kazi”.

Dizzo ambaye pia alidirect video ya Quick Rocka ‘My Baby’, amesema kampuni ya E-media haitakuwepo tena, pia kuanzia sasa atakuwa akisimama mwenyewe kama director tofauti na mwanzo kila video ilikua inasomeka majina mawili likiwemo la Sama Jahn.

“one of the changes pia ni hivyo, nitakuwa niko peke yangu kama director”.Alisema Dizzo

Baadhi ya video zingine zilizotayarishwa na Nick Dizzo chini ya E-Media ni pamoja na ‘Love Me’ ya Izzo B, ‘Nafanya’ ya Cyril ft. Jux, ‘Going Crazy’ ya Hemed PHD na ‘Lovely’ ya Gelly wa Rhymes.

Tummoghele ya Izzo B na Nishike mkono ya D-Knob ndio za kwanza kufanywa na Nick Dizzo kupitia Focus Films.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Bora awe busy aache umalaya!

    ReplyDelete
  2. Nyoko wewe mkome nick umeachwa kubali matokeo nyambafffff

    ReplyDelete
    Replies
    1. Haahaaa muhanga mwingine povu limekutooka utadhani mkewe

      Delete

Top Post Ad