WASHABIKI WA SIMBA WALIAIBISHA TAIFA UWANJA WA TAIFA MECHI YA YANGA NA AL AHLY

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Mashabiki wa timu ya Simba wameanza tena kung'oa viti vya kukalia uwanjani hapa na kuwatupia Mashabini wenzao wa Timu ya Yanga waliofurika kwa wingi uwanjani hapa,kwa kile kinachodaiwa kuwa hawataki kukaa nao sehemu moja.lakini kwa hali ilivyo hivi sasa Uwanjani hapa,ni dhahiri kabisa kuwa Mashabiki hao wa Yanga wanaweza kuujaza Uwanja huu hasa kwa jinsi wanavyozidi kuingia Uwanjani hapa.Uongozi wa Vilabu hivi viwili vikubwa hapa nchini unatakiwa kukaa chini na Mashabiki wao na kuwakanya kuhusiana na uharibifu wa Miundombinu wanaoufanya Mashabiki wao katika Uwanja huu wa Taifa,kwani kuendelea kwa vitendo hivi kunazorotesha sana soka letu.Picha zote na Othman Michuzi,Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Mshabiki wa Simba katika picha hii anaonekana aking'oa kiti na kukirusha upande mwingine. Huu sio utaarabu hata kidogo.


 Mashabiki wa Timu ya Simba wakiendelea kuwarushia viti Mashabiki wa timu ya Yanga kabla hata ya mtanange wenyewe kuanza uwanjani hapa.
 Viongozi wa timu ya Yanga wakiwaomba Mashabiki wao kuhama katika eneo hilo na kwenda kujibana katika eneo walilotengewa kama wana Yanga.  
 Mashabiki wa timu ya National Al Ahly wakiongea na Askari Polisi kuomba wakalizuie tatizo hilo.
 Askari Polisi wakiongea na Viongozi wa Timu ya Yanga ili waweze kwenda kuwaomba mashabiki wao waaondoke katika upande ule unaodaiwa kuwa ni wa Mashabiki wa Simba. 
 Mambo yalianza kama masihara huku wengine wakitaniana
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. simba wanatakiwa kufungiwa wasiende uwanjani wamezidi sasa, hawana ustaarabu.

    ReplyDelete

Top Post Ad