Ripoti: Ndege ya Algeria iliyobeba watu 116 imethibitishwa kuwa imeanguka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ndege ya shirika la Algeria iliyokuwa imebeba abiria 116 ambayo awali iliripotiwa kuwa imepoteza mawasiliano kwa zaidi ya dakika 50 imethibitishwa kuwa imeanguka.

Kwa mujibu wa Aljazeera, maafisa wa Algeria wamethibitisha kuwa ndege hiyo iliyokuwa ikisafiri kutoka Burkina Faso kwenda katika mji mkuu wa Algeria, Algiers imeanguka Kusini mwa Mali.

Maafisa wa serikali ya Ufaransa wameeleza kuwa ndege hiyo AH5017 ilipotea kwenye radar katika eneo la Mali baada ya mvua kubwa kunyesha na inaelezwa kuwa vipande vya ndege hiyo vimeanza kuonekana baharini.

Ndege hiyo inayomilikiwa na kampuni binafsi ya Hispania inayofahamika kama Swiftair ilikuwa imebeba abiria 110 na wafanyakazi sita.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad