Diamond Platnumz na Wema Sepetu Mwisho Umefika

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Stori: Imelda Mtema na Gladness Mallya

Mwisho wa reli? Lile penzi lenye taito na mbwembwe nyingi Bongo kati ya sexy lady wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na staa wa Ngoma ya Mdogomdogo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ linadaiwa kufika mwisho baada ya jamaa huyo kumwandikia mwenziye waraka wa kumdhalilisha mtandaoni, Ijumaa Wikienda lina sarakasi nzima.

TUJIUNGE INSTAGRAM
Suala la Wema kukashifiwa liliibuka baada ya wadau mbalimbali ambao ni mashabiki wa Wema wanaojiita Team Wema kuhoji kwenye Mtandao wa Instagram kwamba ni kwa nini Diamond alimtumia Wema kwa kukata mauno jukwaani (hivi karibuni kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza) badala ya kumfungulia biashara ya maana?

“Tujaribuni kumshauri Wema maana tunaona anatumiwa vibaya na huyu Diamond. Haiwezekani ampandishe kwenye majukwaa halafu amkatishe mauno namna ile kama kweli ana nia ya kumuoa,” aliandika mmoja wa wadau ambaye ni mfuasi wa Team Wema.
Team Wema walidaiwa kufungua mjadala huo wa kumshauri ‘msanii wao huyo wa ukweli’ kufuatia kusambaa kwa picha zinazomuonesha Wema akiwa na shosti wake, Aunt Ezekiel Grayson wakikata mauno jukwaani kupitia wimbo wa Diamond wa Mdogomdogo.

WATOA MIFANO YA WAREMBO
Wadau hao walimtaka Wema kuiga mifano ya warembo wenzake waliopita kama Nancy Sumari (2005), Hoyce Temu (1999), Faraja Kotta (2004) na wengine wengi kwa jinsi wanavyojishughulisha na shughuli mbalimbali na kuweza kuendesha maisha yao bila kudhalilishwa majukwaani.

WAKERWA WEMA KUWA MCHEZA SHOO WA DIAMOND
Team Wema walikwenda mbali zaidi kwa kusema kwamba, wanasikitishwa na Wema kutojulikana moja kwa moja anafanya kazi gani ya maana, zaidi ya kuwa na uhusiano na Diamond ambaye anamgeuza kama mcheza shoo wake wa kukata mauno.

DIAMOND AWAJIBU
Baada ya wadau hao kumshauri Wema huku wakihoji baadhi ya mambo ambayo walidai yanamdhalilisha, kupitia mtandao huohuo wa Instagram, Diamond alishindwa kuvumilia ushauri huo uliomgusa na kuamua kuandika waraka wake unaodaiwa kumdhalilisha Wema.
Katika waraka huo, Diamond alieleza kwamba yeye kama yeye huwa anamtimizia Wema mahitaji ya muhimu kama mpenzi wake na suala la kumpa mtaji wa kufanya biashara.

WARAKA WENYEWE:
“Nafikiri ningewaona kweli mna akili na mapenzi ya dhati kwa huyo msanii wenu (Wema) kama mngemshauri apunguze mashoga wapenda anasa na apunguze starehe zisizo na faida, huenda ingemsaidia pesa kuzitumia kwenye kufanya kazi na kuleta maendeleo badala ya kuwapa viwanda vya pombe, mimi kama bwana, wajibu wangu ni kuhakikisha mpenzi wangu anakula vizuri, anavaa vizuri, analala vizuri, na kumuwezesha mtaji wa kufanyia kazi. “Waswahili wanasema mchungaji bora anatakiwa kuhakikisha anampeleka ng’ombe wake kwenye maji safi ila yeye ng’ombe mwenyewe ndiyo anatakiwa aamue kunywa maji!

“Au mnataka nikishampa mtaji niache kufanya na show tena na kuigiza nimuigizie miye? Nisiende studio nikae dukani nimuuzie miye? Ni juhudi zako kwanza! Leo hii hata ningepewa mamilioni ya mamilioni kama nisingekuwa na moyo wa kutaka kujituma na kupenda kufanya kazi yangu, nisingefikia hapa nilipo! Kama nimekuchefua lamba ndimu usitapike.”

WAMGEUKIA DIAMOND
Baada ya waraka huo, mashabiki na wadau waliopo kwenye mtandao huo walimgeukia Diamond kwa kumlaumu kwamba anavyofanya siyo vizuri mbona amemfungulia dada yake Esma Platnumz duka la maana lakini Wema amekuwa akimtumia tu bila faida yoyote?

MARTIN AJIVUA UMENEJA
Kutokana na waraka huo, aliyekuwa meneja wa Wema, Martin Kadinda naye aliandika wa kwake na kutangaza kuachia ngazi ya umeneja kwa mwanadada huyo.

MAMA WEMA AFUNGUKA
Baada ya meneja huyo kubwanga manyanga, wanahabari wetu walimsaka mama mzazi wa Wema, Miriam Sepetu na kumuuliza juu ya mtazamo wake kuhusiana na penzi hilo la mwanaye ambapo alisema kwa sasa penzi hilo limemchosha hivyo anaacha ‘liserereke’.
Alisema kuwa anawaachia wenyewe waendelee kwani ni watu wazima sasa hadi pale atakapohitajika kutoa msaada kama mzazi.

“Jamani sitaki mniweke kwenye masuala ya Wema na Diamond, wao wazungushane wee mpaka watakakoamua wenyewe maana wao ni watu wazima.
“Siwezi kuwaingilia, acha liserereke tuone mwisho wake,” alisema mama Wema.
Jitihada za kumpata Wema zilishindikana baada ya simu yake kuita bila kupokelewa, achilia mbali kutojibu ujumbe aliotumiwa katika Mtandao wa WhatsApp huku mmoja wa marafiki zake akisema kuwa ishu hiyo imemchanganya.

TUJIKUMBUSHE
Penzi la Wema na Diamond limekuwa likigubikwa na sarakasi nyingi kila kukicha. Waliwahi kumwagana kipindi cha nyuma kabla ya kurudiana Oktoba, mwaka jana. Kabla ya kurudiana, kijiti cha penzi la Diamond kilikuwa kikishikiliwa na Mtangazaji Penniel Mungilwa ‘Penny’.
GPL
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

24 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mwacheni mama yetu ( mama wema ) kwenye ujinga huu,
    hana matatizo zaidi ya kutetea mwanae asiingie kwenye mambo yasiyo mazuri
    kwa jamii,wamemdharirisha vya kutosha na sasa inatosha,
    acheni tabia ya kuwa mnampigia simu kwenye mambo ya Wema na Diamond,muone kama ni mamako,ni mamangu,ni dadako,ni bibi yako,ni shangazi yako,MWACHENI JAMANI,TAFADHALI.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hajatetea km wewe nimtu mzma hapo umeshaelewa.sialisemaga wema kuwa mama ake kamuelewa mtu mwenyewe akiambiwa hasikii ndio mama acha liserereke tu km kigodoro mtt akililia wembe mpeee umfurahishe

      Delete
  2. Halafu utadhani hawana wazazi,hivi mamako akiwa anasumbuliwa kwa ushenzi kama huu utajisikiaje?Mwacheni wadaku nyie,njaa yenu ya kutaka kuuza magazeti yenu yasiwafanye mkamkosea heshima mama wema,mama wa mwenzio ni mama yako pia.

    ReplyDelete
  3. Udakuspecially nyinyi ni wasenge sana kila ck tunajadil mambo yaleyae achen ukuma wasenge nyny

    ReplyDelete
  4. mimi namuunga mkono domo inawezekana alishawahi kumpa hela zabiashara wema akazitumiya kwa mambo yake mengine wewe unawona kwa umalaya wema alionawo anaweza kufanya biashara, asizulule akakaye dukani. alfu wakilazimisha kufunga ndoa moja wapo atakuja kuumiya vibaya mno .mimi nawona wema angetulia kidogo akamuomba domo hela akafanya biashara akaacha kuwa namashoga mda wowote. hawo hawo. mambo yakianda sivyo watakucheka kwasababu malaya wenzako wote wacheza flm wewe tu ndio hauna chako na umalaya una muda.owezi kusema utafanya umalaya mpaka kufa haiwezikane kajenge nawewe ahalafu unawonekana kama huna akili lakini huna kwasababu clament alikudanganya akakupa magali akakudanganya kuwa amekununulia nyumba wakati alikuwa mwongo. akini utaki kujifunza. nawo malafiki zako hawana akili wangekuwa nakili wangekushauli ujenge.kama huye azekia atakushauli kitu gani naye hana chake umalaya tu lewo kwako kesho kwake

    ReplyDelete
  5. mama wema maneno aliyamaliza miaka iliyopita ya kua diamond hana mapenzi ya kweli kwa wema ila anamtumia tu.ss wacha tusubiri tutaona nani mama na nani ni mtoto sababu asiyefunzwa na mzazi ulimwengu upo utamfunza.nampenda saana wema ila kwa hili nafikiri mama wema aliliona zamaaani

    ReplyDelete
  6. kweli mdau nakumbuka hiyo ishu ilikua kipindi kile cha wema, diamond na marehemu kanumba mama wema alisema hiyo kitu,ni kweli trusubiri tuone mwisho wake

    ReplyDelete
  7. Lkn kwa nini wema hasomi hzii comment akaona watu wanavyomshauri achukue mfano kwa jokate alivyoachsna na daimond wala hakuyumba ndio anziifi kutafuta na anafanikiwa ndio maana hayumbishwi kama ww kichwa moshi!!!!!

    ReplyDelete
  8. Wema comments anasoma sana,na kujibu anajibu sana,angekuwa na akili angebadilika,ila hana akili.Yeye akili aliyonayo ni kuwaza Almas,aka sukari ya warembo atataka style gani kitandani,basiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.

    ReplyDelete
  9. Wema fanya yako my dear,mwachie penny huyo Domo ,jiendeleze ki. Maisha unapotezewa muda my dear,I SWEAR!!!!!!! Diamond anakuchezea na kukupotezea wakati.na atallaniwa Kama mr nice.

    ReplyDelete
  10. hahahahahahahaaaa leo naona mnaomteteaga wema mnamtetea mama, kwani ile nyumba ya milion 400 iko wapi? hahahahaaa safi sana clement hiyo ndo dawa ya wanaotegemea kuma kuwaweka mjini

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hakuna cha nyumba ya mil 400 wala nini,kila kitu cha Clement kwishneeeeeey.
      anakumbuka mpaka mil.13 alizomtolea kajala,
      anakumbuka pia alizochezea kule china kwenda kubadilisha muonekano wa ngozi.
      Kwani hata ile misaada kwa watoto yatima mara ya mwisho sijui ilikuwa lini,mweee!

      Delete
  11. huyu sukari jmn mbona ameleta hatari kwenye vichwa vya warembo (hasa wanaopenda kick), Ngoma nayo ikivuma saaaana ikivumaaaa, kinachofuata kinafahamika, wewe Diamond ukiwa kama staa tunapenda Sana kazi zako, na tunaona fahari kama hapa jamvini pataandikwa kama una shoo India, una project na mwanamuziki Usher, Davido, Lione Richie, tafuta basi binti uliempenda tulia nae fanya kazi mdg wangu achana na na skendo

    ReplyDelete
  12. Weee acha kabisa nyumba ya milioni 400 nasikia mama ngoma aliwaka, kinoma baada ya kupata taarifa kuwa wema anadai ni Mali yake. Halafu domo si muhongaji cheki wema alivyopauka tanguwarudiane. Sidhani kama hata pesa anayodai kampa wema kufanya biashara ni ya maana ndo maana kichwa maji wema katafuna na shoga zake a kitetegemea fekero dangote atampa zingine sasa hata kama mtaji Kala ndo hata kumpendezesha kama ku change hair styles na mavazi ashindwe kumgharamia au hata hizo pesa Za shopping nazo ananywea pombe? Au Ndo inabidi wapige panga nusu ili aunt ezekiel nae apate kushona sare ya dera for vimattress Yan ni shiiiiiiiideeer na pia petit man wakuache apate kulewa

    ReplyDelete
  13. JAMANI SI MUMUACHE HUYU WEMA NAE APUMUE,WEMA IMEKUWA WEMA,SI YAMEPITA JAMANI?

    ReplyDelete
  14. wema wema cheap aisee uyu.dad naisi mkuma wake umeisha regea jmn kila siku wema wema jmn dada zake wanafanya nn.jmn si wamshauri ivi wema ajazaliwa makaka maan anatia aibu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mdau hunahabari dada zake niwadada wanajielewa wazuri wema chamtoto.wamekaa pembeni kwakuwa dogo top manyota mjuaji hasikii.mbaya zaidi alitembea na bwana wa dada ake marekani huyo bby wa naseeb.nashangaa akichukuliwa dangote mashabiki wake wanatoka mate.bwana wa dada ake alilala nae huyu wema.team makorokocho njooni mchambe mana mnaakili za chupi kama za boss wenu.

      Delete
  15. wema wema cheap aisee uyu.dad naisi mkuma wake umeisha regea jmn kila siku wema wema jmn dada zake wanafanya nn.jmn si wamshauri ivi wema ajazaliwa makaka maan anatia aibu

    ReplyDelete
  16. Kama hakujenga na kufanya investments za maana akiwa na Clement basi kwisha habari yake!
    Hapo kwa Diamond ni kufirwa na uo kuandikwa magazetini kila siku, na kuolewa haolewi ng'o!
    Atajuta fedha alizotupatupa, uzuri unapotea wanaume wa maana wa kumhonga wamehamia kwa Lulu!
    Diamond hela yake ya mawazo na mjanja anaanza kuinvest so hana hela kuuubwa kihivyo ya kuhonga njiwa wake mwenyewe! Wema amejirahisi mno na majuto ni mjukuu!

    ReplyDelete
  17. Joketi Ana bahati alipewaga million kumi cashhhh,anunue Gari ,wema kapewa nini?

    ReplyDelete
  18. Ila mbona wema hapa kati alikua juu sana??? Nakumbuka akamleta omotola, endless production na in my shoez zote c njia za uchakalikaji zile??? Asa cjui imekuaje tena upepo umechange ghafla??? Ila huenda kweli domo hampendi wema ingawa kwa upande mwngn sawasawa, wema katombesha sana jamani kanumba, jumbe, chaz baba, clement, hartman, blue, TID na wengineo... cjui hata hiyo kuma yake opo vipi??? N asa kwa jank ka daimond na pesa alizonazo nafkiri hata ndugu zake hawamuungi mkono kuoa mtu aliewakalia uchi watu zaid ya kumi kwa umri huo... wacha aendelee kumtumia.. h

    ReplyDelete
  19. Alikua juu au clement alimpaisha hlf akamshusha chezea dyudyu ya dangote alikimbilia dyudyu clement akalamba vyake haihuu mfadhili mbuz ule nyama binadamu anamauzi.sasahivi labda apaishwe kimisha na dangote.maana wenzie wanawekeza ye anawaza mashoga nastarehe na dyudyu.

    ReplyDelete
  20. hivi kwanza nianze nahuyo Diamond...kilichokufanya ujiite jina la tajiri mkubwa wa africa n nn....kumchafulia jina amah,,dangote anafanya juhudi za kuhakikisha anawekeza katk kila nchii hapa afrca...wewe unawekeza kwa wanawake tena wasio na kichwa wala miguu,,huna hata lapa linaloitwa kwa jina lako then eti unajiita jina Dangotee.........nije sasa kwa huyo dem wako,,,sikuwahi kuamn kuwa eti hata Mr Blue ashamlala,,,jaman kweeeel...hiv Wema lini utakuwa mtu mzima ukaelewa vile dunia inaenda,,,kwann wewe ni wa kurudishwa nyuma na wanaume while wao wakiendelea na maisha yao hushtukii,,,hiv jipe baaada ya miaka m'4 toka sasa unadhan utakuwa na umbile na sura ipi,,,acha ulimbukeni wa mapenzi wewee....cjuwi hata ilikuwaje hata ukaweza kuwa Miss coz kiwango chako cha elimu nak'dought mnoo amah ukute ulishatembea hata na Lundenga coz yani wewee cjuwi hata nikuiteje.......badilika pesa za wanaume Always n za muda tena n za wakt mamah,,dimond akija kushuka kama huyo TID wako unadhani wewe tutakukuta wapiii.......tafuta vyako mamaaah.....niiishie hapo next time nikichafukwa nitakuja kwenu nyie kina TeamWema ufyokooooo....................PitaHivi.........

    ReplyDelete
  21. jamani mbona hivyo? kamsapoti mpenzi wake kwenye kazi mnachonga hivyo du wabongo ni shiidah! hivi huyo wema ni mtoto mpaka afanyishwe kazi bila kujijua jamani jamanii! he! hizo nisapoti za baby wake akiwa kazini kwani huyo domo si anasteji shoo wake nyie wasenge kweli, na hata akipata pesa kwani anakula na nanani nyie mnaoponda wote matakoo

    ReplyDelete

Top Post Ad