google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Jeshi la Polisi Ladai Kuwashika Watu Walio Muua Mtoto Akizuia Gari la Baba yake Lisiibiwe na Majambazi Hao | UDAKU SPECIAL

Jeshi la Polisi Ladai Kuwashika Watu Walio Muua Mtoto Akizuia Gari la Baba yake Lisiibiwe na Majambazi Hao

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha limewatia mbaroni watu saba wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya wanawake pamoja na uporaji wa kutumia silaha mjini hapa.

Taarifa iliyotolewa kwa waandishi wa habari jana na Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, ilisema kuwa kati ya watuhumiwa hao, wawili walifikishwa mahakamani juzi na kusomewa mashtaka.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, waliokamatwa wanahusika pia na tukio la kumpiga risasi mtoto wa miaka mitatu, Christen Nickson, aliyeuawa wakati akiwazuia wahalifu hao 

wasipore gari la wazazi wake, Agosti 21, mwaka huu.

Kamanda Sabas aliwataja watuhumiwa waliofikishwa mahakamani juzi kuwa ni Japhet Lomnyaki (25), mkazi wa Sakina na Nehemia Kweka (34), mkazi wa Ngaramtoni.

Watuhumiwa wanaoendelea kuhojiwa aliwataja kuwa ni Adam Mussa, maarufu kwa jina la Badi Makonde (30), mkazi wa Majengo, Tito Loomoni (25), mkazi wa Shamsi, Joseph Loomoni (29), mkazi wa Shamsi, Abdallah Maglan (22), mkazi wa Oldadai na Emmanuel Maglan (23), mkazi wa Oldadai.

“Watuhumiwa hao wanadaiwa kuhusika katika tukio la Agosti 21, mwaka huu, lililotokea eneo la Olasite, kwani siku hiyo walikuwa na pikipiki aina ya Toyo na walimjeruhi kwa kumpiga risasi mtoto Nikson na kumuua,” alisema Kamanda Sabas.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Sasa hiyo picha ya bomu hapo inahucikaje??acha upuuzi wewe

    ReplyDelete
  2. r.i.p nickson..

    ReplyDelete

Top Post Ad