Msichana Kupata Mimba Bila Kukusudia ni Uzembe, Mwanaume Asilaumiwe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kumekuwepo na malalamiko toka kwa wasichana kwamba kijana/mwanaume amenipatia mimba na anakwepa matunzo ya mtoto. Jambo la msingi hapa upatikanaji wa mimba mwenye kujilaumu ni msichana kwa kutokuwa makini. Sina maana kutetea wanaume wanaokwepa child support, ila najadili uzembe wa wasichana wengi kutokuwa makini na kushtukia wamepata mimba bila kukusudia.

Kuna mada moja ililetwa hapa  ikijadili jinsi wasichana wasivyo makini katika kutumia kinga (condom) wanapofanya ngono na wapenzi wao isipokuwa mwanaume ndiye ashughulikie. Hii inatoa picha jinsi wasivyo makini. Pengine kubana matumizi kwao kutaka kila kitu ashughulikie mwanaume matokeo it cost them, may be kisaikolijia ni inferiority complex ya wasichana kadhaa, lakini walio wengi wako makini sana.

Siku hizi hata wanandoa hupanga lini wapate mtoto na wanataka watoto wangapi, iweje msichana ajiachie kupata mimba bila makubaliano na mwanaume? Kama mpango ni kuoana kwa nini asihakikishe taratibu za kuoana zinakamilika ndipo wapate mtoto? Siku hizi hata mwanafunzi wa darasa la tano anajua tayari namna gani mimba inapatikana na namna gani awe makini kuepa kupata mimba tokana na elimu ya bayolojia shuleni.

Kuna uwezekano kupata mimba bila kuingiliana na mwanaume, hasa kwa romance s3x ambayo husababisha mwanaume kupata semen ejaculation na ikafika karibu na v@gna au kufikia v@gna wakati mwanamke eneo hilo la vagna liko wet dhahiri semen zinazobaba sperm zitakuwa zimepata reli ya uhakika kuingia ndani iwapo majira ni ya kuangua yai na ute ni ule laini, ukashangaa kwa vipi unapata mimba wakati hukufanya ngono kumbe mchezo wa romance umekubebesha mimba.

Urafiki mitandaoni nao hufanya marafiki kuwa karibu mno na kuzoeana hadi kufikia kufanya miadi ya kukutana na kufanya yale ambayo yanahatarisha kupata mimba tokana na kuhamasishana kwa online romance na hatimaye wakutanapo ni full mzuka wa patashika nguo kuchanika. Nakumbuka kulikuwa na mtandao mmoja wa BONGO  walikuwa na utaratibu wa kukutana ili kujuana na wengi walidandia na kudandiwa kwa mwendo huo wa kujuana hadi kupata watoto kama hawana akili na leo mzazi mmoja peke yake kabeba mzigo. Tuwe makini.

Akina dada jihadharini na mambo haya yafuatayo:
Ijue vizuri kalenda yako ya siku za kushika mimba.
Uelewe ute mzito usioruhusu semen kupenya na ute laini unaoruhusu semen kupenya.
Romance s3x hakikisha umevaa chupi pekee isiyopitisha majimaji kwenye vagna.
Usikubali kufanya ngono bila kinga.
Uwe mwangalifu mpenzio ambaye umemsababishia kupata ejaculation akishika sehemu yake ya siri kidole kikigusa vagna au nyeti yake kugusa eneo au karibu na vagna kuna uwezekana wa kushika mimba.
Jihadhari kulewa usije ukafanya ngono bila akili timamu kesho yake ukajilaumu akili ikikurudia, majuto ni mjukuu.
Usijiruhusu kujenga mazoea ya flirting ambayo yatakufikisha kufanya ngono sababu ya mhemuko wa kuzoeana.

Msichana ndiye mwenye nafasi ya kujiruhusu kupata mimba au kutopata, vinginevyo ni uzembe wa msichana mwenyewe. Hata hivyo inapotokea msichana kupata mimba kisha kuzaa mtoto mwanaume aliyesababisha mimba anawajibika kusaidia kutunza mimba na child support.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mhhh lakini kuna watu wanaobakwa kwa bahati mbaya

    ReplyDelete

Top Post Ad