AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kitendo cha Nagu kusema kuita watu wezi sio vizuri bila kusema kama kuiba ni vizuri ni dhahiri kuwa CCM haina kinyaa tena na wezi, mafisadi wala watu wenye tabia za kutowajibika ktk kazi kama Pinda.
CCM imeshindwa kutetea umma na hivyo kutetea maslahi yake na wanachama wake viongozi pekee huku wanachama wadogo wakiachwa kuishi kwa bahatisha za maisha.
Maneno ya Kibajaji kuwa kumpatia mtu hela haliwezi kuwa kosa, ni kuthibitisha kukosa kwa maadili ndani ya chama mchana kweupe, mtumishi wa umma anapatiwa fedha na mtoa huduma za jamii kwa mikataba ambayo kila siku inabishaniwa kuwa ni ya wiz wizi. Haingii akili mwa mtanzania isipokuwa mwanaccm tu kuwa waziri wa nishati wastaafu na aliopo wapate chochote, ag mstaafu na aliyepo atape chochote, mawaziri kama tibaijuka apate chochote, watumishi wa umma na wengine wa TRA wapate chochote kutoka kwa mtu mmoja bila kujua hela hiyo ni hongo kwa namna fulani. mbona hajagawia watu tu mitaaani? ni wazi wamepewa hela kwa nyazifa zao. na ni rushwa.
Rais yuko kimya, na uozo huu. Serrikali inadai hela ni za mtu binafsi, je iweje ag na cag watoe maelekezo ya kutoa na kukagua fedha za mtu binafsi??? JK tujibu hilo.
Tukishindwa kwa hili basi jamii ya tanzania bila kujali hasara na mwelekeo wa mbele, inapaswa tukatae kwa nguvu zote watu wa namna hii wizi wa namna hii, na matumizi mabaya ya ofisi.
Nawasilisha
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK