Mahakama ilimshindwa Davido, inawezaje kuzuia Escrow Bungeni?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Oktoba 18, mwaka huu, mwanamuziki kutoka Nigeria, David Adedeji Adeleke ‘Davido’ alipanda jukwaani, akatumbuiza na kuondoka kurudi nchini kwao bila kupata usumbufu wowote.

Davido alipanda jukwaa la Fiesta wakati kulikuwa na Amri ya Zuio kutoka Mahakama ya Kisutu, ikiikataza Kampuni ya Prime Time Promotion kumtumia Davido kwenye shoo ya Fiesta kutokana na mgogoro wa kimkataba baina yake na Kampuni ya Times Promotions and Entertainment, vilevile alinyimwa kibali na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata).

Hata hivyo, Davido alipanda jukwaani na hakuna uamuzi wowote wa dharura ambao ulichukuliwa kutoa fundisho kwa wakaidi wa Amri ya Zuio. Ile adhabu ya kudharau mahakama (Contempt) haikufanya kitu.

Ni aibu kubwa kwa taifa letu ambalo linaongozwa na misingi ya sheria na dola. Ni nchi isiyokuwa na dola peke yake ndiyo alichokifanya Davido hapa nchini kinaweza kutokea na kuvumiliwa kana kwamba hakikutokea kitu. Mahakama haikuona aibu hii!

Kama kwa Davido ilitokea hivyo, nitashangaa sana kama bunge litanywea na kuamua kusitisha hoja nzito yenye maslahi mapana kwa taifa. Bunge linaweza kuendelea na kazi yake. Halafu wahusika waendelee kutapatapa mahakamani. Swali; kama kweli ni watu wazuri na walitenda kilicho halali na haki, wasiwasi wa kukimbilia mahakamani wa nini wakati Ripoti ya Escrow haijasomwa?

Jibu ni kwamba wanajua walichokifanya na wanaelewa kilichomo ndani ya Ripoti ya Escrow na wanatambua nini ambacho kinaenda kusomwa na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe, kwa maana hiyo ni waelewa wa kile kinachokaribia kuwapata. Ripoti isomwe, hata wakizuia itavuja na wananchi watachukua uamuzi. Tuache kulinda ufisadi kwa amani yetu na maendeleo ya uchumi wetu.

Mungu ibariki Tanzania.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad