google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Nguvu na Ushawishi wa Lowassa Waongezeka Maradufu | UDAKU SPECIAL

Nguvu na Ushawishi wa Lowassa Waongezeka Maradufu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

*Tafiti Mpya Za Kitaalamu Zadhihirisha Uhalali wake Kisiasa

*Kauli ya Jk yaongezewa nguvu na Tafiti Mpya za PTT

*Kauli ya mjumbe kamati kuu Jerry Slaa Yampa majibu nape na January "Chama chetu lazima kipeleke bidhaa inayohitajika sokoni, inayouzika na inayokidhi haja ya mnunuaji"

*Tafiti zabainisha nguvu ya Wapinzani Wa Lowassa Pinda na Membe, washindwa kutumia System kumzima Lowassa Zaweka wazi ushawishi wa Lowassa Kwa Umma.

Taasisi isiyo ya kiserikali ya Positive Thinkers Tanzania imetoa ripoti yake ya utafiti kuhusu mwanasiasa anayekubalika zaidi na wananchi katika nafasi ya Rais ajaye, Lowassa aongoza na nafasi ya 2 imeenda kwa Dr. Wilbroad Slaa huku Mwigulu Nchemba aking'ara kama kijana aliyeongoza kwa kukubalika kwa kukamata namba 3.

Ifuatayo ni orodha ya wanasiasa waliongia 10 bora na asilimia ya kura walizopata.

1. Edward Lowassa 22.8%
2. Wilbroad Slaa 19.5%
3. Mwigulu Nchemba 10.6%
4. Ibrahim Lipumba 8.9%
5. John Magufuli 6.8
6. Zitto Kabwe 6.7 %
7. Bernard Membe 5.9%
8. Mizengo Pinda 3.2%
9. January Makamba 1.6%
10. Mark Mwandosya 1.2%

Tafiti hizi zimedhirisha nguvu na ushawishi aliyonayo Edward Ngoyayi Lowassa Kama Kiongozi Kwa Jamii na Umma Wa Tanzania kwa Kiwango Cha Asilimia Alichopata Lowassa Ni dhahiri Shahiri Uchaguzi Ukifanyika leo basi ana nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huo.

Hii ni Tofauti na Wagombea wengine ndani ya CCM ambao kama watapitishwa na chama, chama kitalazimika kutumia nguvu kubwa mno ili kupata ushindi na ushindi ambao unaweza ukawa wa asilimia moja tena baada ya uchaguzi kurudiwa ikiwa ni sehemu ya marudio baada ya round ya kwanza kuonekana kutofikia asilimia.

Tafiti hizi zinaipa kauli ya Mh mwenyekiti na Rais wa tanzania Amiri jeshi mkuu nguvu kwani alisema " ikitokea kuna mtu ananguvu ya kutosha na mnamuona anafaa kuwa Rais basi msisite kumshauri agombee, eeh mshawishini tuuh" kwa muda wa week sasa makundi mbali mbali kada na rika mbali mbali kutoka katika kila kona ya tanzania yamekuwa yakijitokeza kwenda kumuomba Lowassa agombee urais.

Kwa Tafiti hizi watu watapata majibu ni nani anafaa na kwa nini mamia ya watanzania wanajitokeza kumshawishi Edward Lowassa Agombee,Alisema hivi karibuni mjumbe wa kamati kuu ndugu jerry silaaa Yakwamba " chama lazima kipeleke mgombea anayekubalika anayeuzika na anayeweza kukipa chama ushindi" kauli hii ilikuwa mwiba na jibu kwa nape aliyewahi kutoa kauli isiyo ya kiungwana kwa kusema chama hakiwezi kumpitisha mgombea asiyesafishika hata kwa dodoki.

Kauli hii inapingwa na takwimu za tafiti za kitaalamu kwamba Lowassa Ni sawa na kiatu kilichokwisha pakwa kiwi ni kazi ya chama kukibrush tuu" pia kauli hii ni jibu linalomjibu January makamba yakwamba Lowassa Alishapita umri wa kufanya siasa ya maigizo tafiti hizi zinaonyesha namna january anatakiwa kukuza siasa yake watanzania Wamfahamu zaidi na apate uhalali wa kisiasa.

Alisema mama Sophia simba mjumbe wa kamati kuu Kumjibu januaru " kama unaona wenzio wanaigiza kwa kutoa pesa ili watu wawashawishi nawe toa pesa tuone kama kuna mtu atakuja kukushawishi"Pamoja na nguvu kubwa ya kibobezi inayotumiwa na wabobezi hawa wawili pinada na membe bado siasa yao imeonekana kukosa uhalali kwa watanzania tafiti za za kitaalamu mara kwa mara zimekuwa sio rafiki kwa pinda na membe kwa takwimu za tafiti kwa chama cha ccm kumpitisha membe au pinda ni sawa na kupeleka KOFIA YA POLICE DUKANI UKAIUZE Nguvu ya Mwigulu Lamerck Nchemba Imeonekana kuwa Kubwa Kuliko Hata Wabobezi hawa wawili wanaotumia ubobezi wao kupitia system ya serekali na dola kushinikiza makundi mbali mbali kuwaunga mkono.

Hivi karibuni kumekuwa na tabiya ya makundi mbali mbali yanayopewa na kupokea vitisho kutoka kwa wabobezi hawa wawili kwa kosa la kutumia uhuru wao na Dhamira yao njema ya kumshawishi edward atangaze nia na agombee urais.

UKIUWA KWA UPANGA NAWE UTAULIEA KWA UPANGA, TAFITI HIZI ZINAONYESHA SI RAHISI KUZUIYA MKUKI KWA SHUKA
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

6 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mie namkubali king Edward, sasa nyie city council jiandaeni na kazi mutakayo pewa na huyu jamaa ya kusafisha miji nchi nzima kuwe peupe kama Singapore au dubai

    ReplyDelete
  2. Lowasa damdam

    ReplyDelete
  3. Ahhaaaaah wapi! they are the same people.. anakuja kula kama wenzake,, haji kutawala

    ReplyDelete
  4. Ni Lowasa wengine photocopy

    ReplyDelete
  5. Lowasa ndio habari ya mjini kwa sasa.Hakuna mtu wa kumzuia.Anapendwa na wengi.

    ReplyDelete

Top Post Ad