Askofu Pengo akaza uzi, Asema Hawezi Badili Msimamo wake "Waacheni Waumini Wafanye Maamuzi yao Wenyewe Juu ya Kupiga Kura ya Ndio Ama Hapana"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo amesema msimamo wake kuhusu Katiba Inayopendekezwa uko pale pale na ametaka wanaoamini alichosema, wasambaze ujumbe wake kwa wengine.

Akizungumza na Chama cha Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA) hivi karibuni, Askofu Pengo alitoa wito kwa waumini kuachwa huru wafanye maamuzi yao wenyewe juu ya kuipigia kura ya ndiyo au hapana Katiba Inayopendekezwa badala la kushinikizwa na viongozi wa dini kuipigia kura ya ‘hapana’ katiba hiyo.

Aidha, amesema kamwe hawezi kubadili kile alichosema kwani ni ukweli anaouamini na alishaweka hilo wazi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. asiyekujua nani Kadinali? kauli zako nyingi kama si zote ni za kujipendekeza tu kwa serikali hata kama wanafanya makosa...anyway.. siyo kosa lako ndivyo mlivyo nyie wa kutoka Rukwa aka sumbawanga

    ReplyDelete
  2. anataka tuseme kweli kisha tukamatwe......hana lolote

    ReplyDelete
  3. Wote magaidi tu wa Garsia hmna lolote, kama ni free country kwa nini watu wasie free kufanya yao, kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe,,,,,, waachwe wana TZ wachague wenyewe.

    ReplyDelete
  4. HUYU NAE MWIZI TU HANA LOLOTE

    ReplyDelete

Top Post Ad