Kitila abainisha madhaifu mawili ya Zitto Kabwe Katika Uongozi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Prof anachambua pamoja na mambo mengine , madhaifu ya Zitto Kabwe na kushauri apatiwe mda wa kujirekebisha aweze kuwa kiongozi wa kitaifa, mapungufu hayo kwa maneno yake mwenyewe Proffessor:
Pengine udhaifu mkubwa wa Zitto kama kiongozi upo katika maeneo makubwa mawili.

Kwanza, ni kushindwa kupima maana na matokeo mapana ya kauli zake kabla hajazitoa. Mara kadhaa Zitto amekuwa akitoa kauli ambazo huacha ukakasi mkubwa katika jamii.

Kwa mfano, akiwa katika kampeni za ubunge mwaka 2010 alitangaza kwamba katika awamu ijayo angerudi kugombea urais na siyo ubunge tena.

Zitto alitoa tangazo hili huku akijua kwamba chama chake kilikuwa na mgombea urais na kwamba kauli kama ile ingeweza kupunguza imani ya wapiga kura kwa mgombea wa chama chake kwa kuonyesha kwamba asingeshinda na pengine alikuwa hafai.

Pili, baadhi ya kauli za Zitto huonyesha kwamba ni kiongozi anayechokozeka kirahisi.

Kwa mfano, alipomwagiwa ‘upupu’ na Tundu Lissu mapema mwaka huu kwamba alikuwa amehongwa magari na Nimrod Mkono, Zitto alitoa kauli ya haraka tata kwamba, yeye asingekufa kama alivyokufa Chacha Wangwe (“Chacha died, I won’t”).

Hii ni kauli tata kwa sababu inatoa taswira kwamba pengine Chacha Wangwe hakufa kwa ajali kama inavyojulikana bali aliuawa na watu ndani ya chama chake.

Pili, kwamba yeye asingekufa kama Wangwe inaweza kutoa taswira kwamba Zitto ana nguvu za ziada za kumkinga na kifo.

Eneo la pili la udhaifu wa Zitto lipo katika mahusiano ya kimapenzi yasiyoeleweka kwa mtu mwenye dhamana ya uongozi. Zitto amekuwa akihusishwa na wasichana kadhaa maarufu hapa nchini ambao maadili yao kindoa yanatia shaka katika mazingira ya Kitanzania.

Inapokuja katika mahusiano ya kimapenzi, Zitto hujisahau kabisa kwamba yeye ni kiongozi mkubwa katika jamii pamoja na kwamba ana haki zake kama binadamu.

Pengine hili ndilo eneo ambalo Zitto ameshindwa kujitofautisha na wanasiasa wenzake hapa nchini, ambao wengi wao nao uadilifu wao katika eneo hili ni wa mashaka.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hacha upuuzi huyo zito anakubalika hata akigombea hapa mz hatashida kwa kishindo

    ReplyDelete

Top Post Ad