AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Pengine udhaifu mkubwa wa Zitto kama kiongozi upo katika maeneo makubwa mawili.
Kwanza, ni kushindwa kupima maana na matokeo mapana ya kauli zake kabla hajazitoa. Mara kadhaa Zitto amekuwa akitoa kauli ambazo huacha ukakasi mkubwa katika jamii.
Kwa mfano, akiwa katika kampeni za ubunge mwaka 2010 alitangaza kwamba katika awamu ijayo angerudi kugombea urais na siyo ubunge tena.
Zitto alitoa tangazo hili huku akijua kwamba chama chake kilikuwa na mgombea urais na kwamba kauli kama ile ingeweza kupunguza imani ya wapiga kura kwa mgombea wa chama chake kwa kuonyesha kwamba asingeshinda na pengine alikuwa hafai.
Pili, baadhi ya kauli za Zitto huonyesha kwamba ni kiongozi anayechokozeka kirahisi.
Kwa mfano, alipomwagiwa ‘upupu’ na Tundu Lissu mapema mwaka huu kwamba alikuwa amehongwa magari na Nimrod Mkono, Zitto alitoa kauli ya haraka tata kwamba, yeye asingekufa kama alivyokufa Chacha Wangwe (“Chacha died, I won’t”).
Hii ni kauli tata kwa sababu inatoa taswira kwamba pengine Chacha Wangwe hakufa kwa ajali kama inavyojulikana bali aliuawa na watu ndani ya chama chake.
Pili, kwamba yeye asingekufa kama Wangwe inaweza kutoa taswira kwamba Zitto ana nguvu za ziada za kumkinga na kifo.
Eneo la pili la udhaifu wa Zitto lipo katika mahusiano ya kimapenzi yasiyoeleweka kwa mtu mwenye dhamana ya uongozi. Zitto amekuwa akihusishwa na wasichana kadhaa maarufu hapa nchini ambao maadili yao kindoa yanatia shaka katika mazingira ya Kitanzania.
Inapokuja katika mahusiano ya kimapenzi, Zitto hujisahau kabisa kwamba yeye ni kiongozi mkubwa katika jamii pamoja na kwamba ana haki zake kama binadamu.
Pengine hili ndilo eneo ambalo Zitto ameshindwa kujitofautisha na wanasiasa wenzake hapa nchini, ambao wengi wao nao uadilifu wao katika eneo hili ni wa mashaka.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
HAFAI
ReplyDeleteHacha upuuzi huyo zito anakubalika hata akigombea hapa mz hatashida kwa kishindo
ReplyDelete