Linex:Sijui Nani Gundu Gani Kila Nikiachana na Mwanamke Anakuwa Adui Yangu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Sunday Mangu ‘Linex’, amesema tangu ameanza kujihusisha katika mapenzi hajawahi kuachana na mwanamke yeyote bila ya kuwa maadui.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Linex alisema haoni sababu ya kuwa hivyo kwasababu hakuzaliwa pamoja na mwanamke huyo lakini anashangaa imekuwa ikimtokea hivyo.

Alisema ni vizuri kumfanya mpenzi wako wa zamani awe rafiki yako wa karibu ili kuweza kubadilishana mawazo na sio kununiana kuwa kama paka na panya.

Ukweli toka nimejua kumpenda mtoto wa kike au kuwa kwenye uhusiano sijawahi kuachana na mtu alafu mahusiano yanapokwisha yule mtu asiwe adui yangu,” alisema.

Sijawahi kujua uzuri wa kumfanya mpenzi wangu wa zamani awe rafiki yangu wa karibu ninachomaanisha ni kuwa hatukuzaliwa pamoja na leo hatuko pamoja basi sitaki kuwa na uadui na wadada ambao nishawahi kuwa na uhusiano nao tuwe marafiki ,” alisema Linex.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad