Mwanasheria Alberto Msando aeleza jinsi sheria ya makosa ya mtandaoni itakavyowapeleka jela wanaopenda kutukana Instagram

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwanasheria maarufu nchini, Alberto Msando amesema sheria mpya ya makosa ya mtandaoni itakula kwa wengi.

Msando ameiambia Bongo5 kuwa utekelezaji wa sheria hiyo si mgumu kama wengi wanavyodhani na infact wengi wataenda jela. “Ili sheria itekelezeke huhitaji kushtaki watu wote,” amesema Msando. “

“Huwezi ukakamatwa wewe umemtukana Albert ukasema na Abdalah alimtukana naye akamatwe. Ukikamatwa wewe tunaanza na wewe. Kwahiyo ukimuona mwenzio amefungwa miezi sita, miaka saba, miaka mitano, amelipishwa faini, definitely utaacha.”

“Kwasababu kazi ya sheria ni kwanza kumrekebisha mtu kwa njia ya adhabu na pili kumsababisha mtu aepuke kufanya jambo kitu fulani. Inapopitishwa ukiona watu wa kwanza wa pili kweli imetekelezeka, kuna watu wataacha zile tabia maake watajua sasa hapa ni tatizo. Na umeangalia kabla hata haijatumika watu wanakuambiwa ‘tutukane ya mwisho mwisho kabla ya hiyo sheria haijaanza kupitia. Tayari watu wameshajua ni makosa kufanya mbili tatu.”

Msando amewataka watumiaji wa mitandao ya kijamii kuheshimiana na kuitumia kwaajili ya maendeleo na kupata taarifa sahihi.

“Mimi nimeitumia vizuri, nimepata wateja zaidi ya watano wa kazi kubwa tu kwa kupitia mitandao ya kijamii.”

Msikilize hapo chini. Source:Bongo5
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad